Post Top Ad

Post Top Ad

Monday, May 31, 2021

1:29 AM

 Semina ya Siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

          Day 3 ya Semina.

Na Mwalimu Samwel Kibiriti.

Asifiwe Yesu Kristo karibu mwana wa Mungu katika semina ya siku ya leo tena.

MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU UNAGUSWA NA MAMBO YAFUATAYO ( B ):

Tunaendelea pale tulipoishia katika semina ya jana ambapo nilikuonyesha mambo 7 yanayogusa mfumo wako wa maisha ya kila siku. Nataka utambue wazi kwamba ili uwe na maisha mazuri yale Mungu aliyokupangia na kukusudia wakati wa kukuumba ni lazima sana uombee haya maeneo ninayokufundisha kiroho kwasababu yanahusika kila siku kuugusa mfumo wako wa maisha uwe unajua au hujui, ndio maana nikiwa mwalimu wa Neno la Mungu nakufunulia siri hizi na kukupatia maarifa haya ninachotamani Mungu ayageuze maisha yako na uishi katika maisha yako halisi hapa duniani.

( 8 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na nchi ninayoishi.

Mwanzo 12:1-3  Mathayo 12:40 ( Kutoka 12:12; 1:13-14 )

🔶 Nchi unayoishi inayagusa maisha yako ya kila siku kutokana na utendaji kazi wa kiroho wa mazingira ya nchi yenu, nataka ujue kwamba Mungu alimtenga Ibrahimu na nchi yake na kumpeleka nchi nyingine kwasababu kwenye ulimwengu wa kiroho mazingira ya nchi aliyokuwa anaishi Ibrahimu yalishikiliwa na roho za miungu. Ndivyo ilivyo mazingira mengi ya kiroho ya nchi nyingi duniani hayako chini ya utawala wa Mungu katika Yesu Kristo bali yako chini ya miungu na hivyo watu wengi maisha yao yamefungwa kupitia nchi wanazoishi kiroho.

❌Je unajua nchi unayoishi kiroho inafanyaje kazi? Hakikisha unaombea sana nchi unayoishi kila siku mbele za Mungu na kuyafungua maisha yako kutoke kwenye mazingira ya kiroho ya nchi yaliyotumika kuyafunga na kuyakwamisha maisha yako hapa duniani.

( 9 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na Nyumba ninayoishi.

Amosi 3:11-12  Isaya 13:21-22 Kutoka 20:2 Luka 11:20-22

🔶 Nyumba unayoishi inahusika sana kiroho kila siku kugusa mfumo wako wa maisha na wako watu ambao maisha yao yamefungwa kwenye nyumba wanazoishi au walizowahi kuishi na kwasababu wanadamu wengi wanaamiji kwamba jambo la nyumba nila kimwili shetani na miungu wamefanikiwa kuyafunga maisha yao. Wako watu ambao Mungu husema nao kwenye ndoto kwamba wamefungwa ndani ya nyumba lakini hawaelewi, nisikilize kuota ndoto uko kwenye nyumba za zamani sana au kwenye nyumba uliyowahi kuishi huko nyuma au kutoa ndoto umefungiwa ndani ya nyumba ni ishara za kiroho kwamba nafsi yako imefungwa katika nyumba na huwezi ukafanikiwa kimaisha hadi ufanye maombi ya kujifungua katika hizo nyumba kiroho.

❌Je unajua utendaji kazi wa kiroho wa nyumba unayoishi? Je nyumba unayoishi iko chini ya utawala wa ufalme wa nani? Wewe fikiria unaishi kwenye nyumba ambayo iko chini ya utawala wa ufalme wa shetani/miungu unafikiri maisha yako au maisha yenu yatakuwaje? Lazima kujikuta unaishi kwenye maisha ya umasikini na kutokufanikiwa hata kama unajitahidi kufanya sana kazi, hakikisha unafanya maombi ya nguvu ya kufungua maisha yako na maisha yenu yaliyofungwa kwenye nyumba.

✔️ Kama unahitaji kupata maarifa mengi ya Neno la Mungu kuhusu Nyumba unayoishi nakuomba tafuta kitabu changu nilichoandika kiitwacho PATA MAARIFA YA KIROHO KUHUSU NYUMBA UNAYOISHI. Ndani ya kitabu nimefunua siri nyingi sana kuhusu nyumba na kuweka maombi mengi yatakayofungua maisha yako yaliyofungwa kwenye nyumba, kitabu ni Tsh 8,000 ( Elfu Nane ) tuwasiliane kwa maelezo zaidi.

( 10 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na utendaji kazi wa  Nafsi yangu.

Ayubu 33:18  Zaburi 25:13 Mithali 23:14 Isaya 38:15

🔶 Utendaji kazi wa nafsi yako ndio ulioamua aina ya maisha unayoyaishi sasa hivi, kwasababu nafsi ndio Injini ya maisha ya mwanadamu hivyo Nafsi yako kama imefungwa maana yake maisha yako yamefungwa hata kama hutaki pia kama Nafsi yako imetekwa ujue kwamba maisha yako yemshatekwa na yanaongozwa na mtu mwingine. Kuna watu mnajitahidi sana kufanya kazi na kusoma lakini hamfanikiwi na kufikia viwango vya juu kwasababu kiroho Nafsi zenu zimeshafungwa na kuharibikwa.

❌Je wewe unaujua utendaji kazi wa Nafsi yako kila siku kiroho? Watu wengi hamfanyi tathimini za Nafsi zenu hivyo kujikuta mnaishi tu kiholela ni lazima ufanye sana maombi ya kuifungua na kuikomboa nafsi yako ili iweze kurudi katika utendaji kazi uliokusudiwa na Mungu wakati wa kukuumba na hapo ndipo utayaona na maisha yako pia yakibadilika na kuwa kama vile Mungu alivyokukusudia.

( 11 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na Madhabahu za kiroho.

Waamuzi 6:11-32 Kutoka 17:14-16

🔶 Madhabahu zilizopo kwenye ulimwengu wa roho zinahusika sana kugusa mfumo wako wa maisha ya kila siku inategemea wewe maisha yako rohoni yameshikiliwa na madhabahu ya nani ya Mungu au miungu. Kwa asilimia kubwa sana ya wanadamu maisha yao kiroho yameshikiliwa na madhabahu za miungu ndio maana hizo madhabahu za miungu zimewatengenezea aina ya maisha magumu sana na kushindwa kutoka hapo miaka na miaka.

❌Je wewe maisha yako rohoni yameshikiliwa na madhabahu ya nani? Wengi maisha yao hayajashikiliwa na madhabahu ya Mungu bali miungu hivyo unayo kazi kubwa kama aliyoifanya Gideoni ya kuvunja hizo madhabahu zilizoshikilia maisha yako au maisha yenu rohoni kisha kuyaunganisha maisha yako na madhabahu ya Mungu katika Yesu Kristo.

( 12 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na maagano ya kiroho.

Mwanzo 17:7  Kutoka 23:32  Luka 22:20 Waebrania 9:16-17

🔶 Maagano ya kiroho yamehusika sana na yanazidi kuhusika sana kugusa mfumo wa maisha ya mwanadamu na maagano mengi yanayohusiana na mwanadamu sio maagano ya Mungu bali ya miungu kwa hawa watu kutokea kwenye familia zao na uzao wao na miji yao na nchi zao, hivyo maagano watu wanaokuzunguka wanayoyafanya na miungu migeni yanakuathiri sana kiroho katika maisha yako kama hutajua jinsi ya kuomba na kujiunganisha na agano la Damu ya Yesu Kristo. Wengi maisha yenu yamefungwa kwenye maagano ya miungu rohoni ndio maana mnaishi chini ya ndoto zenu za maisha na kupitia vipindi vigumu sana kimaisha unalo jukumu la kufanya maombi ya nguvu sana.

❌Je wewe kwenye ulimwengu wa roho umeruhusu maagano yapi yahusike na maisha yako? Hakikisha unavunja maagano yote ya miungu yaliyotumika kuyafunga maisha yako kisha uyaunganishe maisha yako kwenye agano la Mungu kupitia damu ya Yesu Kristo.

✔️ Kwa leo semina yetu inaishia hapa tukutane siku ya kesho ya 4 ya Semina ambapo nitakupatia maarifa mengine kuhusu malango ya kiroho. Nakuomba fanyia kazi kwa maombi somo hili la leo.



Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi:

Vodacom +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel +255 785 855785.

Tigo +255 673 784197.

Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com

Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

            Samwel Kibiriti.

Mei 17, 2021

Mbeya Tanzania.

@Kibiriti2021

Naomba washirikishe watu wengine somo hili nao wapokee Maarifa haya ya Neno la Mungu ili maisha yao yafunguliwe na Yesu Kristo.

Saturday, May 29, 2021

12:23 PM

 30 Day Seminar (Christ For All People Church- Mbeya).

DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM.

               Day 2 of the Seminar.

By Master Samuel Kibiriti.

Praise the Lord Jesus Christ son of God almost today for the seminar and God will speak to you and minister to you, today let's learn this;

YOUR DAILY LIFE SYSTEM IS AFFECTED BY THE FOLLOWING (A) :

Genesis 1: 26-27 1 Thessalonians 5:23

🔵 Today I want us to study this area of ​​your lifestyle. As I said yesterday that human life is built on the system of birth and death and within the system of life there are schooling, marriage & work, working, happy or unhappy, crying and laughing etc. so I want to show you areas that affect your lifestyle daily. 

These areas make sure that you pray a lot for your prayers because whether you know it or not these areas affect your daily life system depends on your life being affected positively or negatively depending on what is going on in these areas every day that's why I told you to pray hard of God for these areas that affect your daily life system.

(1) My system of life is affected by spiritual gates .

Deuteronomy 28:52 Lamentations 4:12

🔶 Spiritual gates touch your life system of everyone you live on earth and there are so many people whose lives do not move forward and do not succeed in achieving their goals because they are spiritually locked in spiritual gates. Many Christians do not pray for their spiritual gates and thus find enemies passing by and closing their lives.

❌ How do your spiritual gates work in relation to your life? How do the gates of the family you live in and the country you live in and the city you live in work every day in relation to your life?

Make sure you pray hard for the spiritual gates that touch your daily life, but remember before you pray for the spiritual gates you must dedicate yourself to God as I taught you in yesterday's seminar.

✔️ For more information on spiritual gates, please get a copy of my book I wrote called GOD'S DEDICATION PRAYERS SPIRITUAL GUIDELINES THAT AFFECT YOUR LIFE, in this book I have taught you many things that will be helpful to you. The book is Tsh 8,000 (Eight Thousand) contact me for more information.

(2) My way of life is affected by the spiritual Heavens .

Deuteronomy 28:23 Matthew 3: 16-17

🔶 The spiritual heavens are involved in a very large percentage every day touching your life system on earth and there are so many things that are happening in your spiritual heavens and those things have caused your life to be closed and you find yourself living in suffering here on earth. There are people whose lives are locked in their spiritual heavens and there are families and cities and countries the lives of the people in it are locked in their spiritual heavens.

❌ How do your spiritual heavens work every day? What things are going on in your spiritual heavens? I want you to realize that whatever is going on in your spiritual heavens must be reflected in your life here on earth.

Make sure you pray fervently for your spiritual heavens every day and open your closed life in the spiritual heavens as well as open the lives of your children and siblings.

(3) My lifestyle is affected by the spiritual atmosphere where I am .

Ezekiel 10: 1 Daniel 10: 1,13,20

🔶 The spiritual atmosphere is very much involved every day to touch your daily life system that you live on earth, so you need to pray for the spiritual atmosphere where you live because if the devil and the gods succeed in keeping your spiritual atmosphere where you live there are so many things they will do to prevent your answers. of prayer and causing things to go wrong in your life as God intended.

❌ Who is holding the spiritual atmosphere in your area? Make sure that you make a lot of prayers to open the spiritual atmosphere and fight against all the spirits working in the spiritual atmosphere where you live and work.

(4) My lifestyle is affected by Land performance .

Genesis 4: 10-12 Jeremiah 22: 29-30

🔶 The work that is in the ground you are trampling on and living is very much involved in your daily life system, there are people whose lives are locked in the ground but some are facing various wars whose source is the land and some of you are made by the land. and session and failure in what they do in their lives.

❌ How does the land you walk on every day and the land where you live work about your daily life? Make sure you go into prayer and pray for the land in its operation and open your life locked in the ground.

(5) My lifestyle is affected by the use of Time .

Ecclesiastes 3: 1 Ephesians 5: 15-17

🔶 Your 24 hour day use is very effective in touching your lifestyle and many people have had a bad life because they are wasting their time foolishly and are not using their time wisely. The act of wasting time destroys your life make sure you make the best use of your daily time because human life is built on time and the purpose of your creation is connected with time so be disciplined and disciplined in the use of your time every day.

❌How do you spend your 24 hour daily? Are you spending your time wisely or are you wasting your time? Make sure you ask God to grant you the wisdom to spend time in harmony with His will so that your life will be better here on earth and you can better serve your purpose to be created by God.

(6) My lifestyle is affected by the dreams I have when I sleep .

Job 4: 12-16 Matthew 27:19

🔶 The dreams you dream every day while you are asleep affect your daily life pattern due to what is going on in your dreams, and there are so many people whose lives are closed and ruined due to dreams they have dreamed and failed to pray before God after those dreams . Listen to every dream you have while you are asleep whether you remember it or do not remember it or understand its meaning or do not understand that those dreams affect your daily life so do not try to ignore and ignore the dreams you dream every day.

❌ How do your daily dreams relate to your daily life? Have those dreams not ruined your daily life? Make sure you pray hard for your dream door every day before God.

✔️ For more information about dreams please get my book I wrote called HOW TO PRAY FOR YOUR DREAM DOOR TO NOT SUFFER IN this book I have set 13 rules to pray and you will receive great knowledge, the book is Tsh 5,000 (Five Thousand) contact me for more information.

(7) My lifestyle is affected by the people around me every day .

Ecclesiastes 13:20; 18:24 Isaiah 43: 4

🔶 The people around you in your life and the people around you are very important to take care of them spiritually because the people around you are very concerned about touching your lifestyle. The right people around you every day of your life because your life needs people but not everyone you have to bring and keep very close to your life.

❌ What kind of people are you surrounded by? What spirit are these people carrying? Make sure you get rid of the bad people around you and ask God to connect you with the right people in your life for your purpose in life.



➡️ Today we live here in the seminar and tomorrow we will continue with other things that touch your life and I ask you for today to do this work that we have learned until tomorrow when we meet.

Contact me at the following numbers:

Vodacom +255 765 867574 (WhatsApp).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

By email address is Pastorkibiriti@gmail.com

I am a Teacher of God's Word of Knowledge

Samuel Kibiriti.

May 16, 2021

Mbeya Tanzania.

@ Kibiriti2021

Share this lesson with other people and receive this knowledge and meet us the next day of the seminar.

2:10 AM

 Semina ya Siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

             Day 2 ya Semina.

Na Mwalimu Samwel Kibiriti.

Bwana Yesu Kristo asifiwe mwana wa Mungu karibu siku ya leo ya semina na Mungu atasema nawe na kukuhudumia, leo tujifunze jambo hili;

MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU UNAGUSWA NA MAMBO YAFUATAYO ( A ):

Mwanzo 1:26-27  1Thesalonike 5:23

🔵 Siku ya leo nataka tujifunze eneo hili la mfumo wako wa maisha. Kama nilivyosema jana kwamba maisha ya mwanadamu yamejengwa katika mfumo wa kuzaliwa na kufa na ndani ya mfumo wa maisha kuna kusoma shule, kuoa&kuolewa, kufanya kazi, kuwa na furaha au kukosa furaha, kulia na kucheka n.k hivyo nataka nikuonyeshe maeneo ambayo yanagusa mfumo wako wa maisha ya kila siku. 

Haya maeneo hakikisha kwamba unayaombea sana kwa maombi yako kwasababu uwe unajua au haujui haya maeneo yanagusa mfumo wako wa maisha ya kila siku inategemea maisha yako yanaguswa kwa namna mzuri au namna isiyokuwa nzuri inategemea na kile kinachoendelea katika maeneo haya kila siku ndio maana nikakuambia omba sana mbele za Mungu kwaajili ya maeneo haya yanayogusa mfumo wako wa maisha ya kila siku.

( 1 ) Mfumo wangu wa Maisha unaguswa na Malango ya kiroho.

Kumbukumbu la torati 28:52 Maombolezo 4:12

🔶 Malango ya kiroho yanagusa mfumo wako wa maisha ya kila unayoyaishi hapa duniani na kuna watu wengi sana maisha yao hayaendelei mbele na hawafanikiwi na kufikia malengo yao kwasababu wamefungwa na kubanwa kiroho kwenye malango ya kiroho. Wakristo wengi hawaombeagi malango yao ya kiroho hivyo kukuta maadui wamepita hapo na kuyafunga maisha yao.

❌ Je wewe malango yako ya kiroho yanafanyaje kazi kuhusiana na maisha yako? Je malango ya familia unayoishi na nchi unayoishi na mji unaoishi yanafanyaje kazi kila siku kuhusiana na maisha yenu?

Hakikisha kwamba unayaombea sana malango ya kiroho yanayogusa maisha yako ya kila siku, lakini kumbuka kabla hujaombea malango ya kiroho ni lazima ujiweke wakfu kwa Mungu kama nilivyokufundisha katika semina ya jana.

✔️ Kwa maarifa makubwa zaidi kuhusu malango ya kiroho karibu ujipatie nakala ya kitabu changu nilichoandika kiitwacho  MAOMBI YA KUWEKA WAKFU KWA MUNGU MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MAISHA YAKO, ndani ya kitabu nimefundisha mambo mengi sana yatakayokuwa msaada kwako kitabu ni Tsh 8,000 ( Elfu nane ) wasiliana nami kwa maelezo zaidi.

( 2 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na Mbingu za kiroho.

Kumbukumbu la torati 28:23  Mathayo 3:16-17

🔶 Mbingu za kiroho zinahusika kwa asilimia kubwa sana kila siku kugusa mfumo wako wa maisha unayoishi hapa duniani na kuna mambo mengi sana ambayo yanafanyika kwenye mbingu zako za kiroho na mambo hayo yamesababisha maisha yako kufungwa na kujikuta unaishi kwa mateso hapa duniani. Kuna watu maisha yao yamefungwa kwenye mbingu zao za kiroho na kuna familia na miji na nchi maisha ya watu waliomo ndani yake yamefungwa kwenye mbingu zao za kiroho.

❌ Je wewe mbingu zako za kiroho zinafanyaje kazi kila siku? Ni vitu gani vinavyoendelea kwenye mbingu zako za kiroho? Nataka utambue kwamba chochote kinachoendelea katika mbingu zako za kiroho lazima kitaonekana katika maisha yako hapa duniani.

Hakikisha unaziombea sana mbingu zako za kiroho kila siku na kuyafungua maisha yako yaliyofungwa kwenye mbingu za kiroho pia yafungue maisha ya watoto wako na ndugu zako.

( 3 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na Anga la kiroho mahali nilipo.

Ezekieli 10:1  Danieli 10:1,13,20

🔶 Anga la kiroho linahusika sana kila siku kugusa mfumo wako wa maisha ya kila siku unayoyaishi hapa duniani, hivyo unatakiwa sana kuliombea anga la kiroho mahali unapoishi kwasababu shetani na miungu wakifanikiwa kulishika anga lako la kiroho mahali unapoishi kuna vitu vingi sana watavifanya ikiwepo kuzuia majibu yako ya maombi na kusababisha mambo kutokwenda sawasawa kwenye maisha yako kama ulivyokusudiwa na Mungu.

❌ Je anga la kiroho mahali unapoishi limeshikiliwa na nani kiroho? Hakikisha kwamba unafanya sana maombi ya kulifungua anga la kiroho na kupambana na roho zote zinazotenda kazi kwenye anga la kiroho mahali unapoishi na kufanya kazi.

( 4 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na utendaji kazi wa Ardhi.

Mwanzo 4:10-12  Yeremia 22:29-30

🔶 Utendaji kazi ulioko ndani ya ardhi unayoikanyaga na kuishi unahusika sana katika mfumo wako wa maisha ya kila siku, kuna watu maisha yao yamefungwa kwenye ardhi lakini wengine wanakutana na vita mbalimbali ambazo chanzo chake ni ardhi pia wako wengine wametengenezewa na ardhi maisha ya kutangatanga na kutokuwa na kikao na kutofanikiwa katika yale wanayoyatenda kwenye maisha yao.

❌ Je ardhi unayoikanyaga kila siku na ardhi mahali unapoishi inafanyaje kazi kuhusu maisha yako ya kila siku? Hakikisha kwamba unaingia katika maombi na kuiombea ardhi kwenye utendaji kazi wake na kuyafungua maisha yako yaliyofungwa katika ardhi.

( 5 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na matumizi ya Muda.

Mhubiri 3:1  Waefeso 5:15-17

🔶 Matumizi yako ya muda wa masaa 24 ya siku unahusika sana katika kugusa mfumo wako wa maisha na watu wengi wamekuwa na maisha mabaya kwasababu wanautumia muda kiujinga hawatumii muda kwa hekima. Kitendo cha kupoteza muda kinaharibu maisha yako hakikisha kwamba unatumia vizuri sana muda wako wa kila siku kwasababu maisha ya mwanadamu yamejengwa katika muda na kusudi la kuumbwa kwako limeunganishwa na muda hivyo kuwa na adhabu na nidhamu katika matumizi ya muda wako kila siku.

❌Je wewe unatumiaje muda wa kila siku wa masaa 24? Unatumia muda kwa hekima au unatumia muda kwa ujinga? Hakikisha unamuomba Mungu akujalie hekima yake ya wewe kuutumia muda sawasawa na mapenzi yake ili maisha yako yawe mazuri hapa duniani na uweze kulitumikia vyema kusudi lako la kuumbwa na Mungu.

( 6 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na Ndoto ninazoziota nikilaa.

Ayubu 4:12-16  Mathayo 27:19

🔶 Ndoto unazoziota kila siku ukiwa umelala zinagusa mfumo wako wa maisha ya kila siku kutokana na kile kinachoendelea katika ndoto zako, na kuna watu wengi sana ambao maisha yao yamefungwa na kuharibiwa kutokana na ndoto walizowahi kuziota na kushindwa kuomba mbele za Mungu baada ya kuota hizo ndoto. Sikiliza kila ndoto unayoiota ukiwa umelala iwe unaikumbuka au huikumbuki au unaelewa maana yake au huelewi ujue kwamba ndoto hizo zinagusa maisha yako ya kila siku hivyo usijaribu kudharau na kupuuzia ndoto unazoziota kila siku.

❌ Je ndoto unazoziota kila siku zimehusikaje na maisha yako ya kila siku? Je hizo ndoto hazijaharibu maisha yako ya kila siku? Hakikisha kwamba unaombea sana mlango wako wa ndoto kila siku mbele za Mungu.

✔️ Kwa maelezo mengi kuhusu ndoto karibu ujipatie kitabu changu nilichoandika kiitwacho JINSI YA KUOMBEA MLANGO WAKO WA NDOTO ILI USITESEKE katika kitabu hiki nimeweka kanuni 13 za kuomba na utapokea maarifa makubwa sana, kitabu ni Tsh 5,000 ( Elfu tano ) wasiliana nami kwa maelezo zaidi.

( 7 ) Mfumo wangu wa maisha unaguswa na Watu wanaonizunguka kila siku.

Mhubiri 13:20; 18:24 Isaya 43:4

🔶 Watu wanaokuzunguka katika maisha yako na uliowaweka karibu nawe niwa msingi sana kuwachunga rohoni kwasababu watu wanaokuzunguka wanahusika sana kugusa mfumo wako wa maisha unayoishi ndio maana usipokuwa makini nanmwangalifu na watu wanaokuzunguka utajikuta maisha yako yanaharibika na tabia yako njema, hivyo hakikisha unamuomba Mungu akuongoze kuwa na watu sahihi wa kukuzunguka kila siku ya maisha yako kwasababu maisha yako yanahitaji watu ila sio kila mtu unatakiwa kumleta na kumweka karibu sana na maisha yako.

❌ Je wewe umezungukwa na watu wa aina gani? Hao watu wamebeba roho gani? Hakikisha unawaondoa watu wasiofaa waliokuzunguka na kumuomba Mungu akuunganishe na watu sahihi kwenye maisha yako kwaajili ya kusudi lako la maisha.

➡️ Kwa leo tunaishi hapa katika semina na siku ya kesho tutaendelea na mambo mengine yanayogusa maisha yako nakuomba kwa leo yafanyie kazi haya tuliyojifunza mpaka kesho tutakapoonana.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi:

Vodacom +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

Kwa email address ni Pastorkibiriti@gmail.com

Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

Samwel Kibiriti.

Mei 16, 2021

Mbeya Tanzania.

@Kibiriti2021

Washirikishe watu wengine somo hili nao wapokee maarifa haya na tukutane siku ya kesho ya semina.




Friday, May 28, 2021

12:31 AM

 30-day seminar (Christ For All People Church- Mbeya).

DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM .

                The basis of the Seminar.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Genesis 1: 1 Deuteronomy 28: 52,55 Exodus 12:23 Isaiah 60:11 Lamentations 4:12 Psalm 24: 7-10

Lord Jesus Christ be praised sons of God I would like to welcome you to this 30-day Seminar aimed at addressing your spiritual gates through prayer before God.

        PURPOSE OF THIS SEMINAR:

This seminar has two main objectives namely

( i ) The first purpose of this seminar is to address the spiritual gates that touch your daily life on earth. There are many gates that touch people's lives every day and make their lives as they are today.

( ii ) The pillar of this seminar is to address your lifestyle. Man's life God has put in order and this system of life begins at birth and dies where there are so many things that happen and meet in his life. Now in this seminar we will have a prayer to address your system of life so that you can live the life that God planned for you when He created you and brought you here on earth.

              Day 1 of the Seminar.

DEDICATION TO GOD FOR DEALING WITH SPIRITUAL DOORS THAT AFFECT YOUR LIFE .

Exodus 32:29 John 17:19

In this first day of the seminar I want us to learn about this dedication to God as you deal with spiritual gates. Remember that before you pray for the spiritual gates of your life be sure to dedicate yourself to God, do not try to fight the spiritual gates without first dedicating yourself to God, because the battle of the gates is so real that you must obey this principle of dedication to God first.

WHY DEDICATE YOURSELF TO PRAYING FOR SPIRITUAL DOORS?

There are various reasons why you should dedicate yourself to God first before you can address the spiritual gates that touch your life and let me show you these reasons here;

{ 1 } When you dedicate yourself to God to pray for doors God will make sure that He protects you in prayer.

Psalm 121: 7 1 Peter 1: 5

🔶 When you dedicate yourself to God when you pray at the gates God will make sure that He protects you so that you do not get hurt and attacked from the various spirits sitting in the gates you are praying for to open your life, so if you want God's protection praying for the gates you must dedicate yourself to God.

{ 2 } As you dedicate yourself to God to pray for doors you will receive instructions from God about praying for the doors used to close your life.

Genesis 35: 1 Exodus 12: 1-51

🔶 As you dedicate yourself to God in praying for spiritual gates, realize that God will give you instructions on what to pray for and do in the gates that have been used to close your life. There are so many people whose lives are locked in spiritual gates now it is difficult for you to recognize those doors but when you dedicate yourself to God to pray for the gates God will give you His instructions through His Spirit and guide you through the closed doors of your life to pray according to God's will for your life. opened.

{ 3 } When you dedicate yourself to God to pray for doors it means you are letting God's altar stand with you in your prayers.

Psalm 43: 4

🔶 Another benefit if you dedicate yourself to God to pray for spiritual gates means that you allow God's altar to stand with you in your prayers that you do to pray for spiritual gates and open your life. So make sure that before you start praying for the spiritual gates you dedicate yourself to God and then begin to make those prayers for your spiritual gates.



CONFESS THESE PRAYERS TO DEDICATION TO GOD :

God the Father in the name of Jesus Christ I repent to you for my sins and the wrongs I have done in my life I ask you to forgive me through the blood of Jesus Christ.

Today according to your word Exodus 32:29 I confess with all my heart that I dedicate myself to you at the altar with the blood of Jesus Christ so that as I pray for these spiritual gates God may protect me and give me your instructions and your altar may stand with me every day of prayer by name. of Jesus Christ. Also all that I will be praying for you in this prayer of the gates I dedicate to your altar by the blood of Jesus Christ Amen.

■ Make sure that every day before you begin your prayer of dedication you dedicate yourself to God and then pray for those doors that you will be led by the Spirit of God to pray for.

✔️ Today we end up here in the Seminar to meet the next day of the Second seminar, make sure you work on today's lesson.


By contacting me you will contact me at these numbers

Vodacom +255 765 867574 (WhatsApp).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

By email address is Pastorkibiriti@gmail.com

I am a Teacher of God's Word of Knowledge

        Samuel Kibiriti.

May 15, 2021

Mbeya Tanzania.

@ Kibiriti2021

Share this lesson with others to meet the next day of the second seminar.


Wednesday, May 26, 2021

1:56 AM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).


KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

                Msingi wa Semina.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Mwanzo 1:1 Kumbukumbu la torati 28:52,55 Kutoka 12:23 Isaya 60:11 Maombolezo 4:12  Zaburi 24:7-10

Bwana Yesu Kristo asifiwe wana wa Mungu napenda kuwakaribisha katika Semina hii ya siku 30 inayolenga kuyashughulikia malango yako ya kiroho kwa njia ya maombi mbele za Mungu.

   LENGO LA SEMINA HII:


Semina hii iko na malengo makubwa mawili yaani

( i ) Lengo la kwanza la semina hii ni kuyashughulikia malango ya kiroho ambayo yanagusa maisha yako ya kila siku hapa duniani. Yapo malango mengi ambayo huyagusa maisha ya watu kila siku na kusababisha maisha yao yawe yalivyo leo.

( ii ) Lango la pilo la semina hii ni kushughulikia mfumo wa maisha yako. Maisha ya mwanadamu Mungu ameyaweka katika mfumo na huu mfumo wa maisha unaanzia mtu anapozaliwa hadi anapofariki ambapo kuna mambo mengi sana hujitokeza na kukutana nayo katika maisha yake. Sasa katika semina hii tutakuwa na maombi ya kushughulikia mfumo wako wa maisha ili uweze kuishi maisha ambayo Mungu amekupangia alipokuumba na kukuleta hapa duniani.

              Day 1 ya Semina.

KUJIWEKA WAKFU KWA MUNGU KWAAJILI YA KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MAISHA YAKO.

Kutoka 32:29 Yohana 17:19

Katika siku hii ya kwanza ya semina nataka tujifunze jambo hili la kujiweka wakfu kwa Mungu unaposhughulikia malango ya kiroho. Kumbuka kwamba kabla hujaombea malango ya kiroho ya maisha yako hakikisha kwamba unajiweka kwanza wakfu kwa Mungu, usijaribu kupambana na malango ya kiroho bila kujiweka wakfu kwa Mungu kwanza, kwasababu vita vya malango ni halisi kabisa hivyo unatakiwa utii hii kanuni ya kujiweka wakfu kwa Mungu kwanza.

KWANINI UJIWEKE WAKFU UNAPOTAKA KUOMBEA MALANGO YA KIROHO?

Kuna sababu mbalimbali zinazokuhitaji kujiweka wakfu kwa Mungu kwanza kabla ya kushughulikia malango ya kiroho yanayogusa maisha yako nami nikuonyeshe sababu hizi hapa;

{ 1 } Unapojiweka wakfu kwa Mungu kuombea malango Mungu atahakikisha kwamba anakulinda ukiwa kwenye maombi.

Zaburi 121:7  1Petro 1:5

🔶 Unapojiweka wakfu kwa Mungu wakati unapofanya maombi ya malango Mungu atahakikisha kwamba anakulinda ili usiweze kupata madhara na mashambulizi kutoka kwenye roho mbalimbali zilizokaa kwenye hayo malango unayoyaombea ili kuyafungua maisha yako, hivyo kama unataka ulinzi wa Mungu ukiombea malango ni lazima ujiweke wakfu kwake Mungu.

{ 2 } Unapojiweka wakfu kwa Mungu kuombea malango utapokea maelekezo toka kwake Mungu kuhusu kuyaombea malango yaliyotumiwa kuyafunga maisha yako.

Mwanzo 35:1 Kutoka 12:1-51

🔶 Unapojiweka wakfu kwa Mungu katika kuombea malango ya kiroho utambue kwamba Mungu atakupatia maelekezo yake ya nini unatakiwa kuomba na kufanya katika malango ambayo yametumiwa kuyafunga maisha yako unayoishi. Kuna watu wengi sana maisha yao yamefungwa kwenye malango ya kiroho sasa ni vigumu wewe kuyatambua hayo malango ila unapojiweka wakfu kwa Mungu kuombea malango Mungu atakupatia maelekezo yake kupitia Roho wake na kukuongoza katika malango yaliyofunga maisha yako ili uyaombee sawasawa na mapenzi ya Mungu kwaajili ya maisha yako kufunguliwa.

{ 3 } Unapojiweka wakfu kwa Mungu kuombea malango maana yake unairuhusu madhabahu ya Mungu isimame pamoja nawe katika maombi yako.

Zaburi 43:4

🔶 Faida nyingine ukijiweka wakfu kwa Mungu kuombea malango ya kiroho maana yake unairuhusu madhabahu ya Mungu isimame pamoja nawe katika hayo maombi yako unayofanya kuyaombea malango ya kiroho na kuyafungua maisha yako. Hivyo hakikisha kwamba kabla hujaanza kufanya maombi ya kushughulikia malango ya kiroho ujiweke wakfu kwa Mungu ndipo baada ya hapo uanze kufanya hayo maombi ya kuombea malango yako ya kiroho.

KIRI MAOMBI HAYA YA KUJIWEKA WAKFU KWA MUNGU:

Mungu Baba kwa jina la Yesu Kristo ninatubu kwako dhambi zangu na makosa yangu niliyoyatenda katika maisha yangu ninakuomba unisamehe kwa damu ya Yesu Kristo.

Leo sawasawa na neno lako la Kutoka 32:29 ninakubali kwa moyo wangu kujiweka wakfu kwako katika madhabahu kwa damu ya Yesu Kristo ili ninapokuwa naombea malango haya ya kiroho Mungu unilinde na kunipatia maelekezo yako na madhabahu yako iweze kusimama pamoja nami kila siku ya maombi kwa jina la Yesu Kristo. Pia wote nitakaokuwa nawaombea kwenye haya maombi ya malango nawaweka wakfu kwenye madhabahu yako kwa damu ya Yesu Kristo Amen.

■ Hakikisha kwamba kila siku kabla hujaanza maombi yako ya malango ujiweke wakfu kwa Mungu ndipo baada ya hapo uombee malango hayo utakayoongozwa na Roho wa Mungu kuyaombea.

✔️ Kwa leo tunaishia hapa katika Semina tukutane siku ya kesho ya Pili ya semina, hakikisha unafanyia kazi somo la leo.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi

Vodacom +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

Kwa email address ni Pastorkibiriti@gmail.com

Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

        Samwel Kibiriti.


Mei 15, 2021

Mbeya Tanzania.

@Kibiriti2021

Washirikishe na wengine somo hili tukutane siku ya kesho ya pili ya semina.

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...