Post Top Ad

Post Top Ad

Monday, February 6, 2017

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.



        AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.
               

Bwana Yesu Asifiwe Rafiki yangu katika Kristo Yesu. Karibu tena siku hii ya Leo ndani ya darasa hili la kupokoea Maarifa.

              { KIPENGELE CHA TANO }

Leo nataka tusongee mbele kidogo katika somo hili tuone Aina ya tano ya Maombi ambayo unatakiwa uyaombe.


KUNA MAOMBI YA KUMUULIZA MUNGU.


Huu ni mfumo mwingine wa maombi ambayo unatakiwa uyafanye mbele za Mungu, yaani unafanya maombi ya kumuuliza Mungu.

Wakristo wengi huwa hawafanyi maombi ya kumuuliza Mungu. Iko faida kubwa sana ya kufanya maombi ya mfumo huu wa kumuuliza Mungu
Ni kwanini ufanye maombi ya mfumo huu wa kumuuliza Mungu?

"Tunafanya maombi haya ya kumuuliza Mungu kwa sababu yako mambo mengi yasiyofaa yanayotuandama kwenye maisha yetu, ambapo hatujuia chanzo cha hayo matatizo au hayo mambo, sasa ni lazima tumwendee Mungu Baba kwa mfumo wa maombi haya kumuuliza kwamba Mungu ni kwanini kuna tatizo hili kwenye maisha yangu? Naye atakujibu na kukueleza chanzo chake."

Ngoja nikuonyeshe mifano ya watu wawili waliofanya maombi ya mfumo huu wa kuuliza,

                         Mfano wa Kwanza:

                               MWANZO 25

21 "Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba".
22 "Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda KUMWULIZA BWANA".
23 "BWANA akamwambia, Mataifa mawili yako tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo".

Hapa unamuona Rebeka alipopatwa na shida ya mimba yake akaenda kumuuliza BWANA, yaani alifanya Maombi haya ya kumuuliza Mungu, na alimuuliza kwamba ni kwanini ile mimba inamsumbua. Na Mungu akamweleza sababu ya mimba hiyo kumsumbua na kumtesa.

Je wewe kuna jambo gani linalokutesa ambalo hujui chanzo cha tatizo hilo?

                          Mfano wa pili;

                          1 SAMWEL 23

2 "Basi Daudi akamwuliza BWANA, kusema, Je! Niende nikawapige hao Wafilisti? Naye BWANA akamwambia Daudi, Nenda ukawapige Wafilisti, na kuuokoa Keila".

Unamuona mfalme Daudi baada ya kuletewa taarifa kwamba Wafilisti wamevamia mji wa Keila na kuiba nafaka za watu, kabla hajaenda kupigana nao alichofanya Daudi ni kwenda Kumuuliza BWANA kwamba Je aende kupigana na Wafilisti au asiende? Na Mungu akamjibu na kumwambia aende kwa sababu atawashinda hao maadui zake.

Inawezekana na wewe iko vita kwenye maisha yako kwenye Ndoa, kazi, biashara, elimu, afya, uchumi, huduma n.k na huelewi chanzo cha hiyo vita sasa unachotakiwa ni wewe kwenda kwa mfumo huu wa maombi na kumuuliza Mungu kwamba "Ni kwanini vita hii imeinuka kwangu? Au kwanini napigana vita na Mimi sipati ushindi?" Ukimuuliza Mungu atakujibu na kukueleza chanzo cha hiyo vita na kukupatia mbinu za kuishinda hiyo vita.

Sijajua wakati unasoma somo hili uko katika hali gani ya kimaisha? Inawezekana yako mambo mengi sana ambayo yanakuandama kwenye maisha yako lakini hujui chanzo cha mambo hayo na umeomba lakini hujapata majibu kamili,

Sasa nakushauri katika Kristo Yesu nenda mbele za Mungu kwa mfumo wa maombi haya ya kumuuliza Mungu, kuhusu chanzo cha hayo matatizo hayo mambo hayo na Mungu atakujibu na kukueleza chanzo chake na atakupatia njia ya kufanya.
Kwa Leo naishia hapa tukutane siku ya kesho, fanyia kazi somo hili la Leo.

*                       Nataka nikueleze jambo hili kwamba mwisho wa wiki hii nitatoa kitabu cha somo hili la AINA TOFAUTI ZA MAOMBI ambapo nitaingia kwa undani sana, na kufundisha Aina nyingi sana za maombi ambayo unatakiwa uyafahamu na kumuomba Mungu."

Neema ya Mungu Baba ikuhifadhi.
Kwa mawasiliano nami utanipata kwa simu hizi

Voda 0765 867574
Tigo 0673 784197
Airtel 0785 855785

Asante sana kwa kujifunza somo hili.


mimi ni mwlm Samwel Kibiriti.

@Kibiriti 2017, February 6.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...