Post Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 28, 2017

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.




Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo karibu tena leo katika somo letu hili ili upokee maarifa.

KIPENGELE CHA SABA.

KUNA MAOMBI YA KUDAI HAKI ZAKO MBELE ZA MUNGU.

Huu ni mfumo mwingine wa maombi ambayo unaweza kuyafanya mbele za Mungu ambayo ni maombi ya kudai zile haki zako ambazo shetani na ufalme wake wamezizuia ili usiwe nazo.

   ziko haki zako nyingi sana ambazo kwenye ulimwengu wa roho shetani inawezekana kabisa amekuibia na kukufichia, ambazo sasa unatakiwa uanze kuzidai na kuzirudisha.

ngoja nikuonyeshe kwa mfano ili uweze kunielewa.

{ i } Uzima na Uponyaji ni haki yako kama ni mtoto wa Mungu, soma Yakobo 5:13-15, Isaya 53:5, 1Petro 2:24.

{ ii } Kuwa na Amani na furaha ni haki yako, soma Zaburi 122:7,8 119:165, Malaki 2:5

{ iii } Kuolewa na kuoa ni haki yako, soma Isaya 34:14, Mwanzo 2:18

{ iv } Kuzaa watoto kwenye ndoa yako ni haki yako, soma Kutoka 23:26, Zaburi 127:3

{ v } Kutokuharibika kwa mimba ni haki yako, soma Kutoka 23:26


{ vi } Kujifungua pasipo kufanyiwa operesheni ni haki yako, Soma Isaya 66:9

{ vii } Kufanikiwa kiuchumi ni haki yako, soma Waefeso 1:3, 2Wakorintho 8:9, Kumb 8:18


{ viii } Kuwa na ulinzi wa Mungu kila siku ni haki yako, soma 1Petro 1:5

{ ix } Kufanikiwa kibiashara ni haki yako, soma Isaya 48:17, Zaburi 32:8, Kumb 28:5,12

{ x } Kuishi maisha marefu ni haki yako, soma Ayubu 5:26, Kutoka 23:26, Zekaria 8:4  n.k

hizo ni baadhi tu ya haki zako ambazo Mungu anakutaka uzipate kwenye maisha yako wewe ukiwa kama mtoto wake.

je wewe unazo hizi haki zako kwenye maisha yako? au tayari shetani na ufalme wake wa giza wameshakunyanganya haki zako hizo? kama umeshapokonywa hizi haki zako na hauko nazo kwenye maisha yako ni lazima uingie kwenye maombi na kumuomba Mungu ili akurudishie hizo haki zako kwenye maisha yako.

kwa mawasiliano nami utanipata kwa;

 simu za mkononi ni

vodacom 0765 867574
Tigo   0673 784197
Airtel  0785 855785

kwa Email ni Pastorkibiriti@gmail.com



 

mimi ni mwalimu Samwel Kibiriti.


unaweza kujipatia kitabu chako cha somo hili la AINA TOFAUTI ZA MAOMBI kipo wasiliana nami kwa simu namba hizo au kwa Email hiyo, naweza pia kukutumia mahali popote pale ulipo duniani.

           @kibiriti 2017, Marchi 1 

No comments:

Post a Comment

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...