Post Top Ad

Post Top Ad

Saturday, February 4, 2017

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI



AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

Bwana Yesu asifiwe Rafiki yangu katika Kristo Yesu karibu tena siku ya Leo ndani ya chuo chetu hiki cha maarifa ya kiroho, ili tupokee siri hizi.

{ KIPENGELE CHA PILI.}

Jana tuliangalia aina ya maombi ambayo ni maombi ya kulalamika naamini somo hilo la Jana limefanyika baraka kwako, na kama na wewe ulikuwa unaomba huku unalalamika najua kwamba umeshaanza kubadilika.

Tusongee mbele kidogo Leo tena.


KUNA MAOMBI YA KUOMBOLEZA.

Katika aina za maombi nataka ufahamu kwamba kuna maombi ya kuombeleza ambayo unaweza kuyafanya mbele za Mungu na Mungu akaingilia kati jambo hilo unaloliombea.

        YEREMIA 9

"17 BWANA wa majeshi asema hivi, Fikirini ninyi, mkawaite wanawake waombolezao, ili waje; mkatume na kuwaita wanawake wenye ustadi, ili waje;"

"18 na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujuke maji".

Soma na mstari wa 20-21.

Tunamuona Mungu anawatafuta wanawake Waombolezaji ambao wanatakiwa wafanye haraka kuingia kwenye haya maombi ya kuomboleza na anasema pia wawafundishe na binti zao kuomboleza na kila jirani alie mbele zake kwasababu mauti imepandia kwenye nyumba zao.

     Kwahiyo unaona kwamba kuna jambo baya limeingia kwenye nyumba za hawa wanawake na Mungu anawataka waombe maombi ya kuomboleza kutokana na kile kitu kibaya kilichoingia ndani ya nyumba zao.

✔ Unaweza kumwendea Mungu kwa kufanya maombi haya ya kuomboleza kutokana na mambo ambayo ni chukizo unayoyaona ndani ya kanisa, ndani ya familia, ndani ya mji n.k

Sio tu kwamba wanawake ndio wanaotakiwa kufanya haya maombi ya kuomboleza hapana hata wanaume nao wanatakiwa kufanya maombi haya ndio maana Biblia ikasema "Na wafanye haraka na kutuombolezea, ili macho yetu yachuruzike machozi, na kope zetu zibubujike maji"
Kwahiyo tunahitaji kwenda mbele za Mungu kufanya maombi haya ya kuomboleza kutokana na maovu yanayoendelea kutendeka na tunayashuhudia kwa macho yetu na kuyasikia, hebu tuimimine mioyo yetu mbele za Mungu kwa kuomboleza na kumsihi Mungu asamehe haya yanayoendelea kwenye kanisa, familia, koo, miji, serikali n.k ambayo ni chukizo mbele za macho yake.

           YOELI 1

"13 Jikazeni mkaomboleze, enyi makuhani; Pigeni yowe, enyi wahudumu wa madhabahu; Njoni mlale usiku kucha katika magunia, Enyi wahudumu wa Mungu Wangu; Kwa kuwa sadaka ya unga na sadaka ya kinywaji Zimezuiwa katika nyumba ya Mungu wenu"

"14 ......iteni kusanyiko la dini, Wazee na wakusanye wenyeji wote wa nchi; Waende nyumbani kwa Bwana, Mungu wenu, Na kumlilia BWANA"

Naomba usome hiyo Yoeli Yote katika sura hii ya kwanza.

✔ Unamuona Mungu anazuia sadaka zisije kanisani na kuwataka makuhani yaani wachungaji na wahudumu wote wa madhabahu yake wafanye maombi haya ya kuomboleza na kulala usiku kucha kwenye madhabahu kwa sababu mvua ameizuia na matokeo yake wakulima wameshindwa kupanda na mifugo inakufa yenyewe kwa kukosa malisho.

Kwahiyo yako mambo ambayo yanatokea ambayo Mungu akiyatazama hayamfurahishi kabisa sasa nani wa kuyaombea? Ni Mimi na wewe twende mbele za Mungu tuomboleze na kumsihi asamehe huo uovu na dhambi anazozitazama, na tukiomba kwa Imani Mungu Baba atasamehe.

            YOELI 2
"12 Lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni Mimi kwa mioyo yenu Yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea".

Hii ni aina ya Maombi ambayo Roho Mtakatifu anaweza kukuongoza kuyaomba haya maombi ya Kuomboleza na wewe ingia na kuomboleza mbele za Mungu na kumsihi asamehe na kuingilia kati jambo hilo, naye atakujibu.

 ➤ Tuwapate wapi Wanawake na Wanaume watakaoomboleza mbele za Mungu?

➤ Tuwapate wapi vijana wakiume na wakike watakaoomboleza mbele za Mungu?

Kwaajili ya kanisa, nchi, miji, familia, koo,? Wako wapi?

Roho Mtakatifu akuwezeshe kusimama mbele za Mungu kufanya maombi haya ya Kuomboleza mahali ulipo.

Kwa Leo naishia hapa tukutane tena siku ya kesho ambapo nitakuonyesha aina ya tatu ya Maombi.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi

Vodacom 0765 867574.
Tigo 0673 784197.
Airtel 0785 855785.


KAULI MBIU MWAKA 2017

( 1 ) Acha dhambi.
( 2 ) Yesu Kristo anakuja.
( 3 ) Ishi katika maisha ya Utakatifu kila siku.

      

 Mimi ni Mwalimu Samwel Kibiriti Rafiki yako katika Kristo Yesu.

            @Kibiriti 2017, February 2.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...