Post Top Ad

Post Top Ad

Tuesday, February 28, 2017

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.




Shalom wana wa Mungu karibu sana ndani ya darasa kwa siku hii ya Leo. Naamini utapata maarifa Leo tena.


{ KIPENGELE CHA SITA }.

KUNA MAOMBI YA KUNG'OA KILICHOPANDWA NA SHETANI KWENYE MAISHA YAKO.

Haya ni maombi ambayo yanahusika na kung'oa vitu au mbegu za uovu zilizopandikizwa kwenye maisha yako na shetani na vitu hivyo hukutesa kwenye maisha yako.

Katika Ulimwengu wa roho upande wa giza kuna vitu vingi sana ambavyo havifai wanavyowapandikizia wanadamu kwenye miili yao na nafsi zao,

Unaweza kumkuta mtu amepandikiziwa roho mbalimbali mfano magonjwa, matatizo, mikosi, madeni, kushindwa, ulevi, uzinzi/uasherati, tabia mbaya n.k, hizi ni baadhi tu ya roho ambazo unaweza kupandikiziwa na zinakutesa sana sana kwenye maisha yako.

                                        MATHAYO 15

"13 Akajibu, akasema, kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa"
.
Unamuona Bwana Yesu anasema kwamba kila pando ambalo hajalipanda Baba yake wa mbinguni lazima ling'olewa, hii ikiwa na maana kwamba yako mapando ambayo yamepandikizwa na shetani ndani ya mtu, na yanatakiwa kung'olewa kwa njia ya maombi.

                                     MATHAYO 13

"25 Lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake".

Unaona kwamba shetani anaweza kupanda vitu vyake katikati ya maisha ya mwanadamu.

Ni kuulize wewe umepandikwa vitu gani maishani mwako na shetani? Au shetani amewapandikizia vitu gani watoto wako? Au amepandikiza nini kwenye familia na ukoo wenu?

Unaona kwamba unayokazi ya kumuomba Mungu na kung'oa chochote kile kilichopandikizwa ndani yako na shetani, wachawi, waganga wa kienyeji, roho za mizimu, maadui n.k

Kwa Leo naishia hapa tukutane siku ya kesho tena tukiendelea na somo hili.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa simu

Voda 0765 867574.

Tigo 0673 784197.

Airtel 0785 855785.


KAULI MBINU MWAKA 2017.

( 1 ) Acha dhambi.

( 2 ) Yesu Kristo anakuja.

( 3 ) Ishi katika maisha ya Utakatifu kila siku.





Mimi ni mwalimu Samwel Kibiriti Rafiki yako katika Kristo Yesu.


                                   @Kibiriti 2017, February 7.

No comments:

Post a Comment

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...