Post Top Ad

Post Top Ad

Friday, July 28, 2017

MAOMBI YA ULINZI.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana.

karibu tena ndani ya blog hii uweze kupokea maarifa haya ya kiroho.




{ KIPENGELE CHA NANE }

Kuna Maombi ya Ulinzi.

Haya ni maombi ambayo unatakiwa sana kumuomba Mungu kwa sababu katika dunia hii tunayoiishi tumezungukwa na adui yetu mkuu shetani pamoja na wajumbe/ vibaraka vyake ambao ni wachawi, waganga wa kienyeji, mapepo, majini, mizimu, maadui n.k 

    kwahiyo ni lazima umuombe Mungu kila siku ili akulinde na kulinda familia yako/yenu, kuwalinda watoto wako, kulinda mali zako n.k

                        AYUBU 1

9 Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, je! Huyo Ayubu yuamcha BWANA bure?

10 Wewe hukumzingira kwa ukigo/ukuta pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.

Hapa unayakuta ni mazungumzo kati ya Mungu na Shetani wakati Shetani ametokea huku duniani Mungu akamuuliza Shetani kwamba je amemuona huyo mtumishi wake Ayubu, na Shetani akamjibu Mungu kwamba amemzunguzia ulinzi Ayubu kwahiyo kutokana na ule ulinzi kwa Ayubu na nyumba yake na mali zake ulimfanya asiweze kumshambulia na kumpiga Ayubu.

  Kwahiyo sasa unamuona Shetani anamshawishi Mungu auondoe ule ulinzi wake kwa Ayubu na nyumba yake na mali zake ili aweze kumshambulia na kumpiga, ndio maana Mungu alipomuondolea Ayubu ule ulinzi wake akapata nafasi ya kumpiga na kumshambulia.

   Kwahiyo sasa unatakiwa sana umuombe Mungu ulinzi wake katika maeneo yote ya maisha yako yaani muombe Mungu akulinde wewe mwenyewe, alinde mali zako, alinde watoto wako, alinde wazazi wako, alinde nyumba yako, ayalinde masomo yako n.k ili shetani na wachawi na waganga wa kienyeji na mapepo na majini na roho za mizimu zisiweze kukushambulia.

   Hakikisha usiku na mchana unamuomba Mungu ulinzi wake kwenye kila eneo la maisha yako.

    Kwa mawasiliano nami utanipata kwa simu namba hizi:


Vodacom +255 765 867574.


Tigo         +255 673 784197.


Airtel       +255 785 855785.


kwa Email utanipata kwa   Pastorkibiriti@gmail.com


blogsport: Samwel Kibiritiministry.blogsport.com


July 28, 2017.


Mwalimu Samwel Kibiriti.




                                

3 comments:

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...