Post Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 29, 2017

MAOMBI YA KUMKUMBUSHA MUNGU.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.


Shalom karibu tena tuendelee kujifunza somo hili la aina tofauti za maombi.



{ KIPENGELE CHA TISA }.

Kuna Maombi ya Kumkumbusha Mungu.

Haya ni maombi pia ambayo unatakiwa umuombe Mungu yaani ni mfumo wa kumuomba Mungu kwa kumkumbusha kwa yale aliyokuahidi kwamba atakutendea kwenye maisha yako lakini amekawia kukupatia.

  Inawezekana kabisa ni kweli Mungu amekuahidi ahadi nyingi kwamba atakutendea kwenye maisha yako lakini bado hizo ahadi hazijadhihilika katika maisha yako, kwahiyo unachotakiwa ni kumwendea Mungu kwa mfumo huu wa maombi ya kumkumbusha kwamba Mungu uliniahidi kwamba utanitendea jambo Fulani lakini bado hujanitendea leo nakuja mbele zako kukukumbusha Baba ili unitimilizie jambo hilo kwenye maisha yangu.

                               Isaya 43

26 Unikumbushe; na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.

   Mungu anasema tumkumbushe, sasa anaposema kwamba tumkumbushe haina maana kwamba amesahau Mungu hapana ila anachotaka ni kuona kwamba unaouhitaji ndani ya moyo wako wa kumuona Mungu anatimiza zile ahadi alizokueleza/kukuahidia kwahiyo unapomkumbusha Mungu maana yake anaona kwamba kumbe ndani ya moyo wako unamtaka yeye akitimizie hizo ahadi kwenye maisha yako.

    Nitahitaji usome kitabu cha MALAKI 3:13-18 utaona watu waliokuwa wanamtumikia Mungu wanasemezana maneno magumu sana mbele za Mungu kwamba hakuna faida ya kumtumikia Mungu ndipo akawajibu na kuwaambia kwamba “Ndipo wale waliomcha BWANA waliposemezana wao kwa wao. Naye BWANA akasikiliza, akasikia; na kitabu cha Ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha BWANA, na kulitafakari jina lake”.

Unaona kule mbinguni Mungu anacho kitabu cha Ukumbusho kwahiyo unapomuomba Mungu maombi haya ya kumkumbusha maana yake unamuomba Mungu arudi kwenye hicho kitabu chake cha ukumbusho na aangalie zile ahadi alizokuahidia kwamba atakutendea kwenye maisha yako.

  Ukisoma pia kwenye kitabu cha Isaya 38:1-6 wakati Hezekia alipokuwa mgonjwa na kupewa taarifa kwamba atakufa aligeuka ukutani na kumkumbusha Mungu na Mungu akamsikia na kukumbuka mambo aliyowahi kuyatenda huko nyumba kwenye ufalme wake.


     Ndio maana kuna kipindi cha maisha kinafika unachotakiwa ni kuingia kwenye maombi haya ya kumkumbusha Mungu kwamba Mungu kumbuka mambo niliyofanya kwenye ufalme wako na Mungu ataenda kwenye kitabu hicho cha ukumbusho na kuangalia utumishi wako naye atakujibu na kukutendea au kukuvusha mahali pagumu sana kimaisha.

   Mungu akubariki sana tukutane tena siku ya kesho.

kwa mawasiliano nami utanipa kwa simu hizi:

vodacom +255 765 867574.

tigo          +255 673 784197.

Airtel       +255 785 855785.

Kwa Email ni  Pastorkibiriti@gmail.com

July 29, 2017.


                     Mwalimu Samwel Kibiriti.


No comments:

Post a Comment

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...