Chuo Cha Maarifa ya Kiroho

Post Top Ad

Post Top Ad

Thursday, May 9, 2024

3:15 PM

 Madhabahu ya Maarifa ya Neno la Mungu:

VITA YA UZAO KATI YA SHETANI NA MWANADAMU.

Mwanzo 3:15 Matendo 13:23 Yohana 19:30

Bwana Yesu Kristo asifiwe mwana wa Mungu napenda kukukaribisha katika somo hili naamini kwamba litakuwa msaada mkubwa sana maishani mwako.

( Sehemu ya Kwanza ).

🔶 Kuna vita kwenye ulimwengu wa roho kati ya Shetani na uzao wa mwanadamu na vita hii imesababisha madhara makubwa sana katika maisha ya wanadamu ndani ya uzao. Inawezekana maisha unayoyaishi sasa hivi yamekuwa hivyo sababu ya hii vita iliyopo kwenye uzao wenu, sasa katika somo hili leo na kesho tutaona sababu za kiroho zinazomfanya Shetani kupambana na uzao wako au uzao wenu kisha tutaona tunawezaje kuishinda hii vita maishani mwetu.

FAHAMU MAMBO YAFUATAYO.

Kuna mambo kadhaa ambayo nataka uweze kuyafahamu kuhusiana na vita hii ya uzao wako au uzao wenu na shetani.


JAMBO LA KWANZA:

Shetani anapoinua vita ya uzao ni kuhakikisha uzao wa mwanadamu haumwabudu na kumtumikia Mungu.

Mwanzo 1:26 Isaya 43:7 Yohana 4:23-24 Kumbukumbu 10:12 Mika 6:8

🔶 Mungu alimuumba mtu kwa mfano wake na sura yake ili aweze kumwabudu na kumtumikia hapa duniani ndio maana mtu aliumbwa katika utukufu wa Mungu na Bwana Yesu akasema kwamba Mungu anawatafuta wanadamu watakaomwabudu katika roho na kweli.

Lakini shetani anapoinua vita ya uzao lengo lake kubwa ni kuhakikisha uzao wa mwanadamu hauishi maisha ya kumwabudu na kumtumikia Mungu ndio maana leo hii ukitazama kwenye uzao wa wanadamu wengi hawamwabudu na kumtumikia Mungu aliye hai aliyewaumba na kuwaleta hapa duniani sababu hii ni vita iko kwenye ulimwengu wa roho katika uzao wao.

🔵 Kumbuka kwamba Mungu anakutaka uishi maisha ya kumwabudu na kumtumikia yeye peke yake hivyo pambana na kuishinda hii vita ya shetani kwenye uzao wenu inayokuzuia usiishi maisha ya kumwabudu na kumtumikia Mungu, tumia Damu ya Yesu na Jina la Yesu Kristo katika kuomba kwako.

Pia kama wewe ni mzazi hakikisha kwamba nyie wazazi na uzao wenu mnaishi maisha ya kumwabudu na kumtumikia Mungu siku zenu zote hapa duniani.

JAMBO LA PILI:

Shetani anapoinua vita ya uzao ni kuhakikisha uzao wa mwanadamu unatembea na kuishi kwenye laana sio Baraka.

Matendo 3:25 Mwanzo 22:18 Kumbukumbu 28:59

🔶 Mungu alipomuumba mtu alimuumba katika Baraka na Mungu alikusudia kwamba kila mwanadamu aliyemleta hapa duniani anaishi katika maisha ya baraka sio maisha ya laana.

Hii vita ya shetani na uzao wa mwanadamu lengo lake ni kuhakikisha uzao wa wanadamu unaishi kwenye laana sio baraka za Mungu ndio maana leo hii unaona katika uzao wa wanadamu wanaishi maisha ya laana na kuteseka sana kimaisha.

🟢 Hivyo hakikisha unaishinda hii vita ya uzao wenu inayokulazimisha kuishi maisha ya laana na kutembea katika laana badala ya kuishi katika baraka tumia Damu ya Yesu na Jina la Yesu Kristo kuishinda hii vita kwenye uzao wenu.

Wewe mzazi na uzao wako hakikisheni kwamba mnaishi katika maisha ya Baraka na kutembea katika Baraka za Mungu sio kukubali kuishi katika maisha ya laana.

JAMBO LA TATU:

Shetani anapoinua vita ya uzao ni kuhakikisha uzao wa mwanadamu haumiliki na kutawala kimaisha.

Mwanzo 12:7, 17:7-8, 22:17, 28:14

🔶 Kumbuka kwamba Mungu amemleta mwanadamu hapa duniani aishi maisha ya kumiliki na kutawala sio kuishi maisha ya kumilikiwa au kutawaliwa lakini shetani ndiye ambaye anasababisha kwenye uzao wa wanadamu waishi maisha ya kutawaliwa na kumilikiwa.

Leo hii ukifuatilia maisha ya wanadamu wengi katika uzao wanaishi maisha ya kutawaliwa na maadui pia wanamilikiwa na roho mbalimbali za giza huu sio mpango wa Mungu kabisa bali hii ni vita katika uzao wenu inayokutazimisha wewe usiishi kabisa maisha ya kumiliki wala usiishi kabisa maisha ya kutawala.

🟡 Unahitajika kuingia kwenye maombi kwa kutumia Damu ya Yesu na Jina la Yesu Kristo kupambana na hii vita na kuishi ya shetani kwenye uzao wenu ili sasa wewe uishi katika uhalisia wa maisha yako ya kumiliki na kutawala hapa duniani.

Mzazi hakikisha wewe na uzao wako mnaishi maisha ya kutawala na kumiliki kwasababu huu ndio mpango halisi wa Mungu aliyewaumba.

➡️ Umekuwa unajiuliza kila wakati kwanini kwenye uzao wenu mnaishi maisha hayo ya mateso na maisha magumu na maisha yasiyofaa nataka ujue kwamba hiyo ni vita kati ya Shetani na uzao wenu na wewe ni lazima ukubali kusimama kwenye ulimwengu wa roho kwa njia ya maombi na Neno la Mungu ili kuishinda hiyo vita.

Nimekuonyesha sababu hizo 3 za muhimu ingawa ziko nyingi ili usiendelee tu kulalamika na kulia bali utambue kwamba uko kwenye vita ya uzao wenu na shetani anahakikisha kila mtu wa uzao wenu anaishi katika maisha ambayo sio ya kwake yale Original ya Uumbaji wa Mungu, hivyo unahitajika kuomba sana.


☑️ Siku yetu ya kesho tunapoenda kuhitimisha somo hili nitakuonyesha namna ambayo tunapata ushindi huu wa vita ya shetani na uzao wetu kupitia Yesu Kristo. Hakikisha tunaungana tena pamoja katika darasa letu hili ndani ya madhabahu huu ya Maarifa ya Neno la Mungu siku ya kesho, ila leo hakikisha unalifanyia kazi somo hili.

🔶 Kwa mawasiliano nami kuhusu Ushauri wa kiroho na Maombezi tumia number hii ya Utumishi +255 765 867574 pia tumia number hii kama Chombo chako cha Sadaka mbele za Mungu kwaajili ya kueneza Ufalme wake pamoja nami kupitia Sadaka zako.

Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa 

      Samwel Kibiriti.

April 29, 2024

Mang'ola Karatu Arusha.

Washirikishe wengine masomo haya kama unavyoyapokea toka kwenye madhabahu hii ili nao wapate Maarifa ya Neno la Mungu.

Tuesday, August 24, 2021

11:39 PM

  30-day seminar (Christ For All People Church- Mbeya).


DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM.


          Day 15 of the seminar.



Senior Pastor Samwel Kibiriti.



Halleluy son of God welcome to our today's seminar where God will minister to us.


DEALING WITH THE DOOR OF YOUR CREATION .


Genesis 1: 26-27; 5: 1-2


HOW TO PRAY FOR YOUR CREATION GATE BEFORE GOD (B) .


In yesterday's seminar I gave you 2 steps to pray for your gate of creation before God. I pray that today I will give you another step in prayer.


STEP THREE TO APPLY :


(3) Ask God to establish His purpose at your gate of Creation .


Psalm 33:11 Proverbs 16: 4a Isaiah 46: 9-10


Alip When God created you He created you for His wonderful purpose and in your purpose He has placed all your life that He planned to live on this earth for the years He planned for you so God intended after He brought you to earth you can now live your life within your creative purpose, but this is not the case in most people's lives.


You need to go into prayer before God to ask Him to establish His purpose at your gate of creation so that through that purpose God standing at that gate will reveal your life that God intended and planned to live. When Satan and the powers of darkness want you to not live your life of purpose they clash and fight you at the gate of creation and you have to pray hard before God that gate of creation for you and your children and your parents and siblings.


STEP FOUR TO APPLY :


(4) Ask God to restore you to your place of life in accordance with His purpose to create you .


Ephesians 1: 4 Genesis 3: 9 Psalm 118: 5 


🔵 For everyone before being created by God there is a place of life that God intended for him on earth and that place is in the spirit world, so you should go before God and ask Him to restore you to your place of life according to His purpose to create you. Many people in the spirit world have been removed from their positions which is why in the physical world things do not go as they should.


Make sure you fight hard spiritually at the gate of your creation and every soul that fights for you in life. Remember the blood of Jesus Christ has the power to restore you to your place of life to use in your prayers that you send before God the Father who created you and brought you here on earth.


FIFTH STEP TO APPLY :


(5) Make sure that you shed the Blood of Jesus Christ daily at your gate of Creation.


Exodus 12:23 Hebrews 12:24 Luke 22:20 Hebrews 9: 19-22


In your prayer for the creation gate of your life make sure that you apply the blood of Jesus Christ to that prayer in that gate because in the blood of Jesus it carries so much work so when you release it to your creation gate or creation gate of your parents or your children or your brothers the blood of Jesus Christ will do a great deal of work if it is to cleanse that gate, to open that gate, to redeem that gate etc.


If you are saved you are a priest before God so you are allowed to use the blood of Jesus Christ, stay in prayer to pray for your spiritual gates using the blood of Jesus Christ and the Name of Jesus Christ.


🔶 I have given you those 5 steps to pray for your gate of creation before God make sure you stay focused on prayer and prayer and God is ready to hear and answer your prayers. After completing this gate of creation in our seminar tomorrow we will enter another gate that I want us to address spiritually through prayer.


✔️ Today our seminar ends here let's meet tomorrow make sure you reflect on today's lesson and apply it prayerfully. I ask you to help me share these lessons with others so that they too may gain this knowledge of God's Word and from the suffering they experience in life.


By contacting me you will find me at these numbers, also use these numbers to thank God for your Offerings through this Seminar at this altar of His service.


Vodacom M-PESA +255 765 867574.


Airtel Money +255 785 855785.


Tigo Pesa +255 673 784197.


Email address is Pastorkibiriti@gmail.com



I am a Teacher of God's Word of Knowledge


            Samuel Kibiriti .


May 29, 2021


@ Kibiriti2021


Jesus Christ is coming back to take His church and make sure you are saved and live a life pleasing to God's heart every day.

11:33 PM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.


          Day 15 ya semina.


Senior Pastor Samwel Kibiriti.


Halleluy mwana wa Mungu karibu katika semina yetu ya siku ya leo ambapo Mungu atatuhudumia.


KUSHUGHULIKIA LANGO LA UUMBAJI WAKO.


Mwanzo 1:26-27; 5:1-2

JINSI YA KUOMBEA LANGO LAKO LA UUMBAJI MBELE ZA MUNGU ( B ).


Katika semina ya jana nilikupatia hatua 2 za kuombea lango lako la uumbaji mbele za Mungu naomba leo nikupatie hatua nyingine za maombi, ninachotamani ni wewe kuingia kwenye maombi ukiwa na ufahamu wa Neno la Mungu kuomba ili Mungu akurudishe katika maisha yako halisi aliyokuandalia wakati alipokuumba.


HATUA YA TATU YA KUOMBA:


( 3 ) Muombe Mungu alisimamishe kusudi lake katika lango lako la Uumbaji.


Zaburi 33:11  Mithali 16:4a  Isaya 46:9-10


🟢 Mungu alipokuumba alikuumba kwa kusudi lake lake njema sana na ndani ya kusudi lako ameyaweka maisha yako yote aliyokupangia kuyaishi hapa duniani kwa kipindi cha miaka aliyokupangia hivyo Mungu alikusudia baada ya kukuleta hapa duniani uweze sasa kuyaishi maisha yako yaliyomo ndani ya kusudi lako la uumbaji, lakini sivyo ilivyo kwenye maisha ya wanadamu wengi wanaishi maisha ambayo hata Mungu anahuzunika moyoni mwake kwasababu ni maisha nje ya kusudi lake la kuwaumba.


Unahitajika kuingia kwenye maombi mbele za Mungu kumuomba alisimamishe kusudi lake kwenye lango lako la uumbaji ili kupitia hilo kusudi la Mungu linaposimama kwenye hilo lango litadhihilisha maisha yako uliyokusudiwa na kupangiwa na Mungu kuyaishi. Shetani na nguvu za giza wakitaka usiweze kuishi maisha yako ya kusudi wanakubana na kupambana nawe katika lango la uumbaji ndio unatakiwa kuliombea sana mbele za Mungu hilo lango la uumbaji la kwako na watoto wako na wazazi wako na ndugu zako.


HATUA YA NNE YA KUOMBA:


( 4 ) Muombe Mungu akurejeshe katika Nafasi yako ya maisha sawasawa na nia yake ya kukuumba.


Waefeso 1:4  Mwanzo 3:9 Zaburi 118:5 


🔵 Kila mtu kabla hajaubwa na Mungu kuna nafasi ya maisha ambayo Mungu alimkusudia hapa duniani na nafasi hiyo ipo kwenye ulimwengu wa roho, hivyo unatakiwa kwenda mbele za Mungu kumuomba akurejeshe katika nafasi yako ya maisha sawasawa na Nia yake ya kukuumba. Watu wengi kimaisha rohoni wameshatolewa kwenye nafasi zao ndio maana kwenye ulimwengu wa mwili mambo hayaendi kama yalivyotakiwa.


Hakikisha unapambana sana rohoni katika lango lako la uumbaji na kila roho zinazopambana nawe kimaisha. Kumbuka damu ya Yesu Kristo ina nguvu ya kukurejesha kwenye nafasi yako ya maisha itumie kwenye maombi yako haya unayoyapeleka mbele za Mungu Baba aloyekuumba na kukuleta hapa duniani.


HATUA YA TANO YA KUOMBA:


( 5 ) Hakikisha kwamba unaachilia Damu ya Yesu Kristo kila siku katika lango lako la Uumbaji.


Kutoka 12:23  Waebrania 12:24 Luka 22:20 Waebrania 9:19-22


Katika maombi yako ya kuombea lango la uumbaji la maisha yako hakikisha kwamba unaitumia damu ya Yesu Kristo kwenye hayo maombi yako katika hilo lango kwasababu ndani ya damu ya Yesu imebeba kazi nyingi sana hivyo unapoiachilia kwenye lango lako la uumbaji au lango la uumbaji la wazazi wako au watoto wako au ndugu zako hiyo damu ya Yesu Kristo itafanya kazi nyingi sana ikiwepo kutakasa hilo lango, kufungua hilo lango, kukomboa hilo lango n.k


Kama umeokoka wewe ni kuhani mbele za Mungu hivyo unaruhusiwa kuitumia damu ya Yesu Kristo, kaa kwenye maombi ya kuombea malango yako ya kiroho ukitumia damu ya Yesu Kristo na Jina la Yesu Kristo.


🔶 Nimekupatia hizo hatua 5 za kuombea lango lako la uumbaji mbele za Mungu hakikisha unakaa sana kwenye maombi na kuomba na Mungu yuko tayari kusikia na kujibu maombi yako. Baada ya kumaliza lango hili la uumbaji katika semina yetu ya kesho tutaingia lango lingine ambalo nataka tulishughulikie rohoni kwa maombi.


✔️ Kwa leo semina yetu inaishia hapa tukutane siku ya kesho hakikisha unatafakari somo la leo na kulitendea kazi kwa maombi. Nakuomba unisaidie kuwashirikisha watu wengine masomo haya ili nao wapate maarifa haya ya Neno la Mungu na kutoka kwenye mateso walionayo kimaisha.


Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi, pia tumia hizi namba kumshukuru Mungu kwa Sadaka zako kupitia Semina hii kwenye madhabahu hii ya utumishi wake.


Vodacom M-PESA +255 765 867574.


Airtel Money +255 785 855785.


Tigo Pesa +255 673 784197.


Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com



Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa


            Samwel Kibiriti.


Mei 29, 2021


@Kibiriti2021


Yesu Kristo anarudi kulichukua kanisa lake hakikisha kwamba umeokoka na kuishi maisha ya kupendezesha moyo wa Mungu kila siku.

Thursday, July 29, 2021

6:13 AM

  30-day seminar (Christ For All People Church- Mbeya).


DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM.


             Day 14 of the seminar.


Senior Pastor Samwel Kibiriti.


Praise the Lord Jesus son of God let us continue with today's seminar.


DEALING WITH THE DOOR OF YOUR CREATION .


Genesis 1: 26-27; 5: 1-2


May I introduce you a little into the seminar of this gate of spiritual creation.


HOW TO PRAY FOR YOUR CREATION GATE BEFORE GOD (A) .


In today's and tomorrow's seminar I want to teach you how you can pray for your creation gate or the creation gates for your children or your parents or siblings before God every day. Because many of you do not pray for the gate of your creation due to lack of spiritual knowledge but through this seminar gives you the insight you will have before God in your prayers.


FIRST STEP TO APPLY :


(1) Pray to God for your life on earth.


1 John 1: 8-10 Ephesians 4:27 Romans 3:23


You need to pray for repentance before God for the life you are living on earth if you need God's help at your creation gate also if you are praying for someone else at His creation gate make sure you ask for repentance before God for him. Remember that sin is what gave the devil the legitimacy to hold your gate of creation or the gate of creation of the one you are praying for and that is why you must begin with a prayer of repentance before God.


SECOND STEP TO APPLY :


(2) Break the spirits of your birth nature that are at work in your gate of creation .


Ezekiel 16: 1-4 John 10:36; 16:21 Ecclesiastes 4:14


🔴 Among the spirits that have caused people to be unable to live their God-ordained life at the time of their creation are the natural spirits of their birth have been standing against the lives of many people spiritually, so you should enter into prayer to break the natural spirits of your birth where they work in your gate of spiritual creation.


The history of most people's births is not very good from the time they were conceived and the nine months they lived in their mothers' wombs and their births and the things they did after birth there are many superstitious and customary circumstances created thus giving legitimacy to various dark spirits and rule over them and guide their spiritual lives and thus find in the physical world they suffer and struggle in daily life and this does not please the heart of God.


🔶 I ask you to make a powerful prayer to break the natural spirits of your birth that work at your gate of creation also break those natural spirits in the lives of your children and your parents and siblings working in their gate of creation. Make sure you open your life too which was bound by the natural spirits of your birth in the name of Jesus Christ and the great results you will see in your daily life here on earth.


✔️ For today our seminar ends here make sure you work prayerfully this lesson until tomorrow we will meet where I will show you some steps to pray for your gate of creation before God. Please help me to apply this lesson to others so that they can receive this Understanding of God's Word and not continue to live a life of suffering in their lives.


By contacting me you will find me at these numbers, you can also use these numbers to thank God for your Offerings in this altar of His service.



Vodacom M-PESA +255 765 867574 (WhatsApp).


Airtel Money +255 785 855785


Tigo Pesa +255 673 784197


By Email address is Pastorkibiriti@gmail.com


I am a Teacher of God's Word of Knowledge



           Samuel Kibiriti.


May 28, 2021


@ Kibiriti2021


Let's meet at tomorrow's seminar and make sure you serve God in your life with all your strength.

6:09 AM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).


KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.


             Day 14 ya semina.


Senior Pastor Samwel Kibiriti.


Bwana Yesu asifiwe mwana wa Mungu karibu tuendelee na semina ya siku ya leo.


KUSHUGHULIKIA LANGO LA UUMBAJI WAKO.


Mwanzo 1:26-27; 5:1-2


Naomba nikuingize ndani kidogo katika semina ya lango hili la uumbaji kiroho.


JINSI YA KUOMBEA LANGO LAKO LA UUMBAJI MBELE ZA MUNGU ( A ).


Katika semina ya siku ya leo na siku ya kesho nataka nikufundishe jinsi gani unaweza kuombea lango lako la uumbaji au malango ya uumbaji ya watoto wako au wazazi wako au ndugu zako mbele za Mungu kila siku. Kwasababu wengi wenu hamuombei lango la uumbaji wenu kutokana na kutokuwa na maarifa ya kiroho lakini kupitia semina hii inakupatia ufahamu utakaokaa nao mbele za Mungu kwa maombi yako.


HATUA YA KWANZA YA KUOMBA:


( 1 ) Omba toba kwa Mungu kwaajili ya maisha yako unayoishi hapa duniani.


1Yohana 1:8-10 Waefeso 4:27 Warumi 3:23


🟤 Unahitajika kuomba toba mbele za Mungu kwaajili ya maisha yako unayoishi hapa duniani kama unahitaji msaada wake Mungu kwenye lango lako la uumbaji pia kama unamuombea mtu mwingine kwenye lango lake la uumbaji hakikisha unaomba toba mbele za Mungu kwaajili yake. Kumbuka dhambi ndio iliyompatia shetani uhalali wa kushikilia lango lako la uumbaji au lango la uumbaji la huyo unayemuombea ndio maana lazima uanze na maombi ya toba mbele za Mungu.


HATUA YA PILI YA KUOMBA:


( 2 ) Vunja roho za asili ya kuzaliwa kwako ambazo zinatenda kazi katika lango lako la uumbaji.


Ezekieli 16:1-4 Yohana 10:36; 16:21 Mhubiri 4:14


🔴 Kati ya roho ambazo zimesababisha kuwazuia watu wasiweze kuishi maisha yao waliyopangiwa na Mungu wakati wa kuumbwa kwao ni roho za asili ya kuzaliwa kwao zimekuwa zikisimama kinyume na maisha ya watu wengi kiroho, hivyo unatakiwa kuingia kwenye maombi ya kuvunja roho za asili ya kuzaliwa kwako ambapo zinafanya kazi katika lango lako la uumbaji kiroho.


Historia za kuzaliwa kwa watu wengi sio nzuri kabisa kutokea kutungwa kwao mimba na miezi tisa waliyokaa tumboni mwa mama zao na kuzaliwa kwao na vitu walivyofanyiwa baada ya kuzaliwa kuna mazingira mengi ya kishirikina na kimila yamefanyika hivyo kutoa uhalali kwa roho mbalimbali za giza kupata nafasi ya kuwashikilia na kuwatawala na kuongoza maisha yao rohoni na hivyo kukuta katika ulimwengu wa mwili wanateseka na kuhangaika kimaisha kila siku na jambo hili haliufurahishi moyo wa Mungu.


🔶 Nakuomba fanya maombi ya nguvu ya kuvunja roho za asili ya kuzaliwa kwako ambazo zinafanya kazi kwenye lango lako la uumbaji pia vunja hizo roho za asili katika maisha ya watoto wako na wazazi wako na ndugu zako zinazofanya kazi katika lango lao la uumbaji. Hakikisha unayafungua maisha yako pia yaliyokuwa yamefungwa na roho za asili ya kuzaliwa kwako kwa jina la Yesu Kristo na matokeo makubwa utayaona kwenye maisha yako ya kila siku hapa duniani.


✔️ Kwa leo semina yetu inaishia hapa hakikisha unafanyia kazi kwa maombi somo hili mpaka siki ya kesho tutakapokutana ambapo nitakuonyesha hatua nyingine za kuombea lango lako la uumbaji mbele za Mungu. Naomba unisaidie kuwatumia wengine somo hili ili wapokee Ufahamu huu wa Neno la Mungu na wasiendelee kuishi kwa mateso katika maisha yao.


Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi, pia unaweza kutumia hizi namba kumshukuru Mungu kwa Sadaka zako katika hii madhabahu ya utumishi wake.


Vodacom M-PESA +255 765 867574 ( WhatsApp ).


Airtel Money +255 785 855785


Tigo Pesa +255 673 784197


Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com


Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa



           Samwel Kibiriti.


Mei 28, 2021

@Kibiriti2021


Tukutane katika semina ya siku ya kesho hakikisha unamtumikia Mungu katika maisha yako kwa nguvu zako zote.

Thursday, July 22, 2021

11:50 PM

  30-day seminar (Christ For All People Church- Mbeya).


DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM .


           Day 13 of the seminar.


Teacher Samuel Kibiriti.


Christ Jesus be praised son of God almost in today's seminar. Having finished learning about dealing with the gate of the soul I believe that you have received much knowledge and prayed for your soul, today I ask you to take me to another spiritual gate that you need to pray for.


DEALING WITH THE DOOR OF YOUR CREATION .


Genesis 1: 26-27; 5: 1-2


🔶 In the spirit world there is a gate of creation that carries your life that you live here on earth every day. Many people do not have the spiritual awareness of their gate of creation and thus fail to pray daily to pray for their gates of creation and thus cause the devil and the powers of darkness to hold their gates of creation and use them to torment them in their lives and live difficult lives. very contrary to God's plan to create them and bring them into the world.


WHY DOES SATAN FIGHT AGAINST THE GATE OF HUMAN CREATION? .


There are so many spiritual reasons why the devil will fight you at your gate of creation or fight your children, your parents, your siblings, or your spouse in their gate of creation, now as a teacher of God's Word of knowledge I ask you to keep me in your heart a few reasons here to realize the seriousness and importance of praying for your gate of creation or praying for the gates of creation for the people who are around you every day before God.


FIRST REASON :


(1) The gate of creation carries your purpose for God's creation .


Genesis 1:27 Romans 9:11 Proverbs 16: 4 Acts 13:36 Isaiah 46:10


Your gate of creation is the one that carries your purpose of being created by God so the devil is fighting against you in your gate of creation so that you cannot live on earth within your purpose of creation and millions of human beings on earth do not know why God created them and thus fail to recognize their purpose of creation and to find themselves living a life outside of the purpose of their creation.


If Satan and the powers of darkness succeed in holding your gate of creation you will be their captive even if you do not want to because they will not allow you to live within your God-created purpose and also when you try to find your purpose they will attack and fight you hard. Remember there are very serious consequences for you living outside of your God-created purpose because your purpose is what carries your life and the perfect plan of God to create you and bring you into this world so living outside of your purpose is a very great suffering.


❌ Isn't the gate of your creation closed and blocked by the devil and the powers of darkness there so that you cannot live within your purpose of being created by God? You need a lot of prayer help before God to open your gate of creation as well as to open your purpose so that you can live within the purpose and live your real life that God has planned for you in your creation purpose.


SECOND REASON :


(2) The gate of creation carries with me the standards of life that God wanted me to live .

Psalm 37: 7 3 John 1: 2 Psalm 1: 3 Genesis 26:13 Ephesians 1: 3-4



Your gate of creation carries with you the standards of life that God who created you intended to be able to live that life, and if the devil wants to cling to you you cannot live your God-ordained life and reach those standards of life where he fights you spiritually. That is why today so many people live a life that is not theirs and they are also below their standard of living because they are barred there at the gate of creation from being able to live their lives according to the standards of God who created them.


❌ Are you in your life not barred from your gate of creation from being able to live up to the standards God intended for you in life? You need to get more spiritual help at that gate. Make sure you make a prayer for your creation gate and open your life there through the blood of Jesus Christ.


THIRD REASON :


(3) The gate of creation carries with it the kind of work I am supposed to do in my life here on earth .


Psalm 33: 13-15; 104: 23


🔵 In your life here on earth God has not brought you to do all the work you see or do with the people around you. But millions of people, even you, are out of the special work of creation that they are doing here on earth.


When your gate of creation is being held by the devil spiritually among other things he will do to you is to make sure that in your life here on earth you live by doing the work that took you out of heaven to God but he will let you work out of your creative purpose. here on earth. With all the work you do I want you to realize that there is a special work that God wants you to do in your own strength and most of your time because that is what made you come here on earth by God.


❌ Is the work you are doing here on earth the special work that God has brought you to do in your life? You need to get spiritual help before God asks Him to speak to you and show you the work He has sent you to do on earth. There are also people locked in the gate of creation so that they do not do the work that brought them here on earth, make sure you pray before God.


FOURTH REASON :


(4) The gate of creation carries with it the Authority you are to walk with in your life here on earth .


Matthew 28:18 Daniel 7:12


Your gate of creation also carries the authority of your life that you must walk with on earth in the call of God who brought you to earth so that you can serve it because there are many earthly and spiritual circumstances that will fight against you and prevent you from fulfilling your calling. special.


But many people have been deprived of their authority or some have been imprisoned for failing to exercise their authority and those things have been done at their gate of creation. So you should go into prayer and ask God at your gate of creation and ask God to restore your creative power for your life here on earth.


➡️ Today we end here in our seminar, I ask you to work on today's lesson and enter into prayer. In my book PRAYER TO DEDICATION TO GOD SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR LIFE I have described the gate of handicrafts where I taught the effects of working that God has not sent you to do here on earth. Also in my book of THINGS CARRIED INTO YOUR GOD'S CREATION PURPOSE I have explained many things that are within your God-created purpose, make sure you find your copy of these books and other books I have already written that contain God's great Knowledge of the Word of God.


To contact me and offer your offerings at God's altar use these numbers:


Vodacom M-pesa +255 765 867574 (WhatsApp).


Airtel Money +255 785 855785


Tigo Pesa +255 673 784197


Email address is Pastorkibiriti@gmail.com



I am a Teacher of God's Word of Knowledge


            Samuel Kibiriti .


May 27, 2021


@ Kibiriti2021


Your life here on earth will be very rewarding if you trust and trust God in everything you do in your life.

11:39 PM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).


KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.


           Day 13 ya semina.


Mwalimu Samwel Kibiriti.


Kristo Yesu asifiwe mwana wa Mungu karibu katika semina ya siku ya leo. Baada ya kumaliza kujifunza kuhusu kushughulikia lango la nafsi naamini kwamba umepokea maarifa mengi na kuombea nafsi yako, leo naomba nikupeleke katika lango lingine la kiroho unalotakiwa kuliombea.


KUSHUGHULIKIA LANGO LA UUMBAJI WAKO.

Mwanzo 1:26-27; 5:1-2


🔶 Katika ulimwengu wa roho kuna lango la uumbaji ambalo limebeba maisha yako unayoishi hapa duniani ya kila siku. Watu wengi hawana ufahamu wa kiroho kuhusu lango lao la uumbaji na hivyo kushindwa kufanya maombi kila siku kuombea malango yao ya uumbaji na hivyo kusababisha shetani na nguvu za giza kushikilia malango yao ya uumbaji na kuyatumia kuwatesa katika maisha yao na kuishi maisha magumu ya shida na taabu sana kinyume na mpango wa Mungu kuwaumba na kuwaleta hapa duniani.


KWANINI SHETANI ANAPAMBANA NA LANGO LA UUMBAJI LA MWANADAMU?.


Kuna sababu nyingi sana za kiroho zinazomfanya shetani apambane na wewe katika lango lako la uumbaji au apambane na watoto wako, wazazi wako, ndugu zako, au mke/mume wako katika lango lao la uumbaji, sasa nikiwa mwalimu wa Neno la Mungu la maarifa naomba nikuwekeee ndani ya moyo wako sababu chache hapa ili utambue uzito na umuhimu wa kuombea lango lako la uumbaji au kuombea malango ya uumbaji ya watu wanaokuhusu kila siku mbele za Mungu.


SABABU YA KWANZA:

( 1 ) Lango la uumbaji limebeba Kusudi lako la kuumbwa na Mungu.

Mwanzo 1:27 Warumi 9:11 Mithali 16:4 Matendo 13:36 Isaya 46:10


Lango lako la uumbaji ndilo limebeba kusudi lako la kuumbwa na Mungu hivyo shetani anapambana nawe katika lango lako la uumbaji ili usiweze kuishi hapa duniani ndani ya kusudi lako la kuumbwa na Mungu na mamilion ya wanadamu wengi waliopo hapa duniani hawajui kwanini Mungu aliwaumba na hivyo kushindwa kutambua kusudi lao la kuumbwa na kujikuta wanaishi maisha yaliyo nje ya kusudi la uumbaji wao.


Shetani na nguvu za giza wakifanikiwa kushikilia lango lako la uumbaji wewe utakuwa mateka wao hata kama hutaki kwasababu hawatakuruhusu uweze kuishi ndani ya kusudi lako la kuumbwa na Mungu na pia utakapojaribu kutafuta kusudi lako watakushambulia na kupambana na wewe sana. Kumbuka kuna madhara makubwa sana ya wewe kuishi nje ya kusudi lako la kuumbwa na Mungu kwasababu kusudi lako ndilo limebeba maisha yako na ule mkakati kamili wa Mungu kukuumba na kukuleta hapa duniani hivyo ukiishi nje ya kusudi lako ni mateso makubwa sana sana.


❌ Je katika lango lako la uumbaji hujabanwa na kuzuiliwa na shetani na nguvu za giza hapo ili usiweze kuishi ndani ya kusudi lako la kuumbwa na Mungu? Unahitaji msaada mkubwa wa maombi mbele za Mungu kufunguliwa kwa lango lako la uumbaji pia kufunguliwa kwa kusudi lako ili uweze kuishi ndani ya kusudi na kuyaishi maisha yako halisi ambayo Mungu amekupangia ndani ya kusudi lako la uumbaji.


SABABU YA PILI:

( 2 ) Lango la uumbaji  limebeba viwango vyangu vya maisha niliyotakiwa na Mungu niyaishi.

Zaburi 37:7  3Yohana 1:2  Zaburi 1:3  Mwanzo 26:13 Waefeso 1:3-4


Lango lako la uumbaji limebeba viwango vyako vya maisha ambayo Mungu aliyekuumba alikukusudia kuweza kuyaishi hayo maisha, na shetani akitaka kukubana usiweze kuishi maisha yako uliyopangiwa na Mungu na kufikia vile viwango vya maisha mahali anapopambana nawe kiroho ni katika lango lako la uumbaji hapo ndipo vita inapovhezwa. Ndio maana leo watu wengi sana wanaishi maisha yasiyokuwa yao pia wako chini ya viwango vya maisha yao kwasababu wamezuiliwa hapo kwenye lango la uumbaji wasiweze kuyaishi maisha yao kwenye viwango vya Mungu aliyewaumba.


❌ Je wewe katika maisha yako hujazuiliwa kwenye lango lako la uumbaji usiweze kuishi katika viwango vya Mungu alivyokupangia kimaisha? Unahitajika kupata msaada zaidi wa kiroho kwenye hilo lango hakikisha unafanya maombi ya kuombea lango lako la uumbaji na kuyafungua maisha yako hapo kwa damu ya Yesu Kristo.


SABABU YA TATU:

( 3 ) Lango la uumbaji limebeba aina ya kazi ninayotakiwa kuifanya katika maisha yangu hapa duniani.

Zaburi 33:13-15; 104:23


🔵 Katika maisha yako hapa duniani Mungu hajakuleta ufanye kila aina ya kazi unayoiona au inayofanywa na watu wanaokuzunguka nataka ujitambue kwamba Mungu kila mtu aliyemuumba na kumleta hapa duniani kuna kazi maalum ambayo amemuandalia na kumkusudia kila mtu kuifanya kwaajili ufalme wake hapa duniani. Lakini mamilion ya wanadamu hata wewe wako nje ya kazi maalum ya uumbaji wao wanazofanya hapa duniani wengi hufanya kazi ambazo sio zile zilizomfanya Mungu amewaumba na kuwaleta hapa duniani wazifanye kila siku.


Lango lako la uumbaji linaposhikiliwa na shetani kiroho kati ya jambo lingine atakalokufanyia ni kuhakikisha kwamba kwenye maisha yako hapa duniani huishi kwa kuifanya kazi ile iliyokutoa mbinguni kwa Mungu bali atakuacha ufanye kazi nje ya kusudi lako la uumbaji pia atapambana nawe usitambue kabisa kazi uliyotumwa na Mungu kuifanya hapa duniani. Pamoja na kazi mbalimbali unazofanya nataka ujitambue kwamba kuna kazi maalum ambayo Mungu anakutaka hiyo uifanye kwa nguvu zako na muda wako mwingi kwasababu ndio iliyokufanya umeletwa hapa duniani na Mungu.


❌ Je wewe kazi unayoifanya hapa duniani ndio kazi maalum ambayo Mungu amekuleta uifanye kwenye maisha yako? Unahitajika kupata msaada wa kiroho mbele za Mungu kumuomba ili akusemeshe na kukuonyesha kazi aliyokutuma hapa duniani uweze kuifanya. Pia kuna watu wamefungwa katika lango la uumbaji ili wasifanye kazi ile iliyowaleta hapa duniani, hakikisha unaomba mbele za Mungu.


SABABU YA NNE:

( 4 ) Lango la uumbaji limebeba Mamlaka unayotakiwa kutembea nayo katika maisha yako hapa duniani.

Mathayo 28:18 Danieli 7:12


Lango lako la uumbaji pia limebeba mamlaka ya maisha yako unayotakiwa kutembea nayo hapa duniani katika ule wito wa Mungu aliokuleta hapa duniani ili uweze kuutumikia kwasababu kuna mazingira mengi hapa duniani naya kiroho ambayo yatapambana nawe na kukuzuia usiweze kutimiza wito wako ndio maana Mungu alipokuumba akakubebesha mamlaka yako maalum.


Lakini watu wengi wamepokonywa mamlaka zao au wengine wamefungwa wasiweze kutumia mamlaka zao na mambo hayo yamefanyika kwenye lango lao la uumbaji. Hivyo unatakiwa kuingia kwenye maombi na kumuomba Mungu katika lango lako la uumbaji na kumuomba Mungu akurejeshee mamlaka yako ya uumbaji kwaajili ya maisha yako hapa duniani.


➡️ Kwa leo tunaishia hapa kwenye semina yetu, nakuomba fanyia kazi somo la leo na kuingia kwenye maombi. Katika kitabu changu cha MAOMBI YA KUWEKA WAKFU KWA MUNGU MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MAISHA YAKO nimeeleza lango la kazi za mikono ambapo nilifundisha madhara ya kufanya kazi ambayo sio Mungu amekutuma kuifanya hapa duniani. Pia kwenye kitabu changu cha VITU VILIVYOBEBWA NDANI YA KUSUDI LAKO LA KUUMBWA NA MUNGU nimeeleza kuhusu mambo mengi yaliyomo ndani ya kusudi lako la kuumbwa na Mungu, hakikisha kwamba unapata Nakala yako ya vitabu hivi na vitabu vingine nilivyokwisha kuandika ambavyo vimebeba Maarifa makubwa ya Mungu ya Neno la Mungu.


Kwa mawasiliano nami na kutoa sadaka zako kwenye madhabahu ya Mungu tumia namba hizi:

Vodacom M-pesa +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel Money +255 785 855785

Tigo Pesa +255 673 784197

Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com



Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa


            Samwel Kibiriti.

Mei 27, 2021

@Kibiriti2021


Maisha yako hapa duniani yatakuwa ya faida kubwa sana kama utamwamini na kumtegemea Mungu katika kila jambo unalofanya kwenye maisha yako.

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...