Post Top Ad

Post Top Ad

Wednesday, June 16, 2021

5:44 AM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

         Day 10 ya semina.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Bwana Yesu Kristo atukuzwe mwana wa Mungu karibu tuendelee na semina ya siku ya leo.

KUSHUGHULIKIA LANGO LA NAFSI YAKO ( A ).

Zaburi 25:20 Kutoka 32:7 Kumbukumbu 4:16 Hesabu 11:18 Zaburi 7:5  Hesabu 31:50

Baada ya kumaliza kukufundisha kuhusu kupambana na lango la nchi unayoishi na kujifungua kwenye madhabahu za nchi zilizofunga maisha yako, leo nataka tuanze somo hili la lango la Nafsi yako ambapo tutajifunza kwa siku 3 kuhusua lango hili, na Mungu atasema nawe na kuifungua nafsi yako. Wako aatu wengi sana hawajui jinsi nafsi zao zinazofanya kazi kiroho na pia lango hili la nafsi kwa watu wengi limeshikiliwa na nguvu za giza ndio maana nafsi zao zinateseka na kutumikishwa sana kila siku wakiwa katika usingizi na kwenye ndoto bila kupata msaada wa kuwaweka huru.


SABABU YA VITA KATIKA NAFSI YAKO.

Naomba leo nikueleze sababu za vita katika nafsi yako na katika nafsi za watoto wako na wazazi wako na ndugu zako. Kuna vita kubwa sana iliyoelekezwa kwenye nafsi za wanadamu na hii vita imesababisha nafsi nyingi kutokufanya kazi kama vile zilivyoumbwa na Mungu kwenye maisha ya watu. Na wengi hawajui kwanini wanakutana na vita sana kila siku katika nafsi zao, mimi kama mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa naomba nikueleze hizo sababu kibiblia zinazosababisha uko kwenye vita ya nafsi yako kila siku.


                SABABU YA KWANZA:

( 1 ) Nafsi ndio inayoweza kutafsiri Sauti ya roho na sauti ya mwili wako ili vielewane

Wagalatia 5:16-25

🔵 Mungu aliumba roho na nafasi na mwili wako na katika utendaji kazi wa maeneo haya 3 ni kwamba ndani ya roho yako kuna sauti na katika mwili wako kuna sauti hivyo biblia inasema kwamba roho na mwili hazielewani na nafsi yako ndio iliyobebeshwa jukumu na Mungu kutafsiri sauti ya roho na mwili vielewane ili uweze kuyafanya mapenzi ya Mungu katika maisha yako. Nafsi yako inapofungwa kiroho itashindwa kutafsiri sauti ya roho na mwili na hivyo kushindwa kuelewana na kujikuta huishi maisha ya kuyafanya na kuyatimiza mapenzi ya Mungu hapa duniani kila siku.

❌Je nafsi yako inatafsiri sawasawa sauti ya roho na mwili wako na kuelewana katika kuyafanya mapenzi ya Mungu? Hakikisha unafanya maombi ya kuifungua nafsi yako mahali ilipofungwa ili iweze kuwa huru na wewe uweze kuyafanya mapenzi ya Mungu kwenye maisha yako, pia omba Mungu aurejeshe ule uweza wake katika nafsi yako.


                SABABU YA PILI:

( 2 ) Nafsi ndio iliyobeba Maisha yako unayoishi hapa duniani

Ayubu 10:1

Maisha yako unayoishi leo hii yawe mazuri au mabaya chanzo ni nafsi yako wala sio roho yako wala mwili wako kwasababu Mungu alipoiumba nafsi yako ndio aliyoibebesha jukumu la kuongoza maisha yako hapa duniani.  Kwahiyo kwa lugha rahisi tunasema kwamba unavyoishi leo ni matokeo ya nafsi yako ilivyo na inavyofanya kazi rohoni. Huwezi kuwa na maisha unayoyatamani kama nafsi yako imefungwa utakuwa unayasimulia tu hayo maisha pasipo kuyaishi kwa uhalisia hapa duniani hivyo ni jambo la msingi kujua kwamba nafsi yako iko huru au imefungwa ili uweze kuiombea mbele za Mungu.

❌Je maisha unayoyaishi sasa ndivyo Mungu alivyokupangia uwe nayo? Jibu ni hapana kuna maisha mazuri sana wakati Mungu alipokuumba alikuandalia na kukupangia ila kwasababu nafsi yako imefungwa umejikuta huyaishi hayo maisha. Hakikisha unapata msaada wa kiroho kufunguliwa kwa nafsi yako ili uweze kurudi katika maisha yako halisi uliyokusudiwa na Mungu, na muombe Mungu ayarejeshe maisha yako halisi ili uweze kuyaishi hapa duniani kwa kipindi atakachokuweka kuishi.


                       SABABU YA TATU:

( 3 ) Nafsi ndio iliyobeba kiu ya wewe kumtafuta Mungu kwenye maisha yako

Zaburi 42:2 Yohana 7:37 Zaburi 143:6 Yeremia 29:13

Wakristo wengi ndani yao hawana kiu kabisa ya kumtafuta Mungu na kuutafuta uso wa Mungu kwasababu ile kiu imeshaondolewa ndani ya nafsi zao ndio maana unawakuta ni wakristo wa mazoea tu makanisani. Nataka ufahamu kwamba Mungu aliweka kitu kinachoitwa kiu/shauku ndani ya nafsi na kiu hiyo aliyoiweka sio ya kutafuta kufanya kitu chochote kile hapana ameiweka hiyo kiu ili moyo wako umtafute sana Mungu kila siku ya maisha, kwasababu mwenye kuyajua maisha yako ni Mungu pekee wala sio mwanadamu wala kiumbe yoyote yule hivyo unapoweka jitihada kubwa ya kumtafuta Mungu aliahidi kwamba ataonekana kwako.

❌Je ndani ya nafsi yako kuna kiu ya kumtafuta Mungu kila siku? Hakikisha unaingia katika maombi na kuifungua nafsi yako na kumuomba Mungu akurejeshee kiu yake ya wewe kumtafuta yeye zaidi ya unavyotafuta pesa kwani ukimpata Mungu umepata kila kitu katika maisha yako.


                        SABABU YA NNE:

( 4 ) Nafsi ndio iliyobeba Mafanikio ya maisha yako

Zaburi 25:13  3Yohana 1:2

Mafanikio ya maisha yako hayako kwenye roho yako wala hayapo kwenye mwili wako au kwenye utendaji kazi wako sana hapa duniani bali mafanikio yako yamebebwa ndani ya nafsi, kwahiyo nafsi yako ndio inayokuamulia viwango vya kufanikiwa kimaisha hapa duniani. Mtu yoyote ambaye nafsi yake imefungwa hawezi kufanikiwa kimaisha hata kama atajitahidi vipi kufanya kazi hili wengi hawalifahamu. 

❌Mafanikio ya maisha yako yamewekwa na Mungu katika nafsi yako hivyo hakikisha unaombea sana nafsi yako na kuifungua ili uweze kuishi maisha ya mafanikio hapa duniani sawasawa na kusudi la Mungu la kukuumba.


                    SABABU YA TANO:

( 5 ) Nafsi ndio Injini ya kufanya kazi kwa mtu hapa duniani

Mithali 16:26  Zaburi 104:23  Mhubiri 3:13

Injini ya mwanadamu ya kufanya kazi za mikono sio mwili bali ni nafsi yake  na wengi hawafahamu hili ndio maana watu wengi unawakuta wanafanya kazi za mikono kwa kutumia miili yao wakati huo nafsi zao zimefungwa rohoni na kujikuta wanajitahidi kweli kufanya kazi lakini maisha yao hayabadiliki kabisa kila siku. Nafsi yako ndio injini ya kufanya kazi ili kufanikiwa kwenye kazi zako kwahiyo injini inapofungwa hakuna kitu kitasogea kwako. 

Nafsi ndio inayotakiwa ishirikiane na mwili kufanya kazi za mikono kwa pamoja lakini sivyo ilivyo wengi sana mwili ndio unaofanya kazi bila kushirikiana na nafsi ndio maana hawafanikiwi wala kupata matokeo yale waliyokusudiwa kuyapata kupitia kazi zao za mikono. Kufanya kazi kubwa kwa mwili wako huku nafsi yako ikiwa imechukuliwa mateka kiroho ni kujichosha bure bila faida yoyote katika maisha yako ndio leo unakutana na watu wengi wanaolalamika kuteseka na kuchoka kupitia kazi wanazozifanya bila kufanikiwa na kustawi wao wakidhania tatizo ni kazi kumbe tatizo lipo kiroho nafsi zao zimeshafungwa na kuibiwa na kutekwa na maadui.

❌Je nafsi yako inafanya kazi kwa kushirikiana na mwili wako kwa ukamilifu au unatumia mwili peke yake kufanya kazi huku nafsi yako ikiwa kifungoni? Ingia kwenye maombi ya nguvu ya kuifungua nafsi yako katika utendaji kazi wake wa kila siku kwenye maisha yako.


               SABABU YA SITA:

( 6 ) Nafsi ndio iliyobeba Akili na mawazo na fikira

Akili na mawazo na fikira Mungu aliziweka ndani ya nafsi kwahiyo nafsi yako ikibanwa na shetani rohoni ujue akili zako na mawazo yako na fikira zako nazo pia zitakuwa zimebanwa, pia nafsi yako ikitekwa nyara rohoni ujue pia na akili zako zimetekwa na mawazo yako yametekwa na fikira zako  zitakuwa zimetekwa na hivyo kushindwa kutumika sawasawa kama Mungu alivyoviumba na kuziweka ndani yako kwaajili ya maisha yako hapa duniani.

 Aliyeshikilia nafsi yako kwenye ulimwengu wa kiroho ndiye huyo atakayeibana nafsi yako na kuiongoza vyovyote atakavyo yeye na kujikuta huwezi kufanya yale unayotakiwa kuyafanya bali unafanya vitu ambavyo hata wewe na wanaokuzunguka wanashangaa tu kwasababu nafsi yako inaongozwa vibaya tofauti na mapenzi ya Mungu.

🔶 Nimeweza kukuonyesha sababu za kiroho kwanini nafsi yako inakutana na vita ni kwasababu ya vitu ilivyovibeba kwaajili ya maisha yako ya kila siku hapa duniani, hivyo ingia katika maombi na kuiombea kwa nguvu nafsi yako hadi ifunguliwe na kuhuishwa na Mungu. Hii vita ya nafsi yako kama hutapata msaada mkubwa wa kiroho utajikuta na maisha ya kuteseka na kuhangaika tu hapa duniani na hilo sio mpango wa Mungu aliyekuumba na kukuleta hapa duniani. Matatizo makubwa ya maisha ya watu waliyonayo yako kwenye nafsi zao kwasababu haziko sawasawa kiroho kabisa kwenye utendajo kazi.


✔️ Kwa leo semina yetu inaishia hapa tukutane siku ya kesho ambapo nitasema nawe kuhusiana na eneo la akili katika nafsi yako. Nakuomba unisaidie kuwashirikisha watu wengine masomo haya ili wapokee maarifa ya kuwatoa katika mateso wanayopitia kimaisha.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi:

Vodacom +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com



Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

          Samwel Kibiriti.

Mei 24, 2021

@Kibiriti2021

Kumbuka Bwana Yesu anarudi hakikisha kwamba umeokoka na kuishi maisha ya utakatifu huku ukiyafanya mapenzi ya Mungu kwenye maisha yako.

Saturday, June 12, 2021

11:05 PM

 30-day seminar (Christ For All People Church-Mbeya).

DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM .

        Day 9 of the Seminar.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Praise be to Jesus Christ my dear friend in today's seminar.

FIGHT AGAINST THE ALTARS OF THE COUNTRIES THAT CLOSED YOUR LIFE AND YOUR LIFE ( B ) .

Deuteronomy 12: 1-4

In yesterday's seminar I talked to you two things about the altars of the country that apply to your life in the daily world today I want to show you some things let's go together.

PERFORMANCE OF THE ALTAR COUNTRIES ABOUT YOUR DAILY LIFE :

Let's look at other types of work;


                  THIRD THING :

( 3 ) The altars of a country may pass on to you a war from the tribes within the country .

Jonah 1: 8 Revelation 13: 1-2,7 Habakkuk 3: 9 Zechariah 11:10 Revelation 5: 9

There are wars in countries whose source is the altars of the country using the tribes within your country, so the question of knowing the number of tribes in your country and the functioning of those tribes is very important to know spiritually. So there are wars in various areas of your life that you encounter every day whose source is the altars of the country using the tribes within the country.

❌In what country do the altars of the gods in the country use in your country? Make sure that you fight in your prayers to end all the battles you encounter from the altars of the country because of the ethnic groups within the country.


                 FOURTH THING:

( 4 ) The altars of a country can close your life through vows made on those altars for the country in which you live .

1 Kings 8:31 Numbers 30: 2 Matthew 23:20

🔵 There are so many people in the country whose lives are bound by vows made and held in the country every day through the altars of the lands of the gods and those vows involve closing the country and because you live in the country you find yourself harmed and so the vows that take place daily secretly in your country, if you will not be the one to pray for the country and fight those altars you will find your life not thriving in the land due to the oaths of the land.

❌Do you fast every day at the altars of your country? Make sure you fight hard on the altars of your country every day in prayer and open your life and your life so that you can have a good life in the country where you live.


                 FIFTH FACTOR :

( 5 ) Offerings offered on the altars of the gods of our country can bind your life .

Ezra 3: 2 Psalm 118: 27 Judges 6: 11,25-26

There are people's lives in the country tied to sacrifices offered on the altars of the gods, and there are many people offering sacrifices on the altars of the land to close the country you live in and the lives of you citizens in the country, so make sure you fight this. the spirit world.

❌Are you praying to destroy every offering made on the altars of the gods of your country that closed your life? Make sure you open your life to those sacrifices on the altars of the world, and make sure that you are obedient and faithful in giving various offerings to the altar of God in Jesus Christ at all times so that through those sacrifices you offer to God that the altar of God can fight against those altars. lands of the gods.


✔️ We end here for today's seminar to meet tomorrow where we will look at the gate of your soul make sure you apply this lesson daily with your prayers. I also ask you to make sure you share these lessons with other people and other groups so that they will receive this Knowledge of God's Word.

Contact me at the following numbers:

Vodacom-MPESA +255 765 867574 (WhatsApp).

Airtel Money +255 785 855785

Tigo Pesa +255 673 784197

By Email address is Pastorkibiriti@gmail.com



I am a Teacher of God's Word of Knowledge

          Samuel Kibiriti .

May 23, 2021

@ Kibiriti2021

Welcome to the various Knowledge in the Books I have written of the Word of God.

4:47 AM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church-Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

        Day 9 ya Semina.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Asifiwe Yesu Kristo rafiki yangu karibu katika semina ya siku ya leo.

KUPAMBANA NA MADHABAHU ZA NCHI ZILIZOFUNGA MAISHA YAKO NA MAISHA YENU ( B ).

Kumbukumbu la torati 12:1-4

Katika semina ya jana nilizungumza nawe mambo mawili kuhusu madhabahu za nchi zinavyohusika na maisha yako ndani ya nchi ya kila siku leo nataka nikuonyeshe mambo mengine twende pamoja.

UTENDAJI KAZI WA MADHABAHU ZA NCHI KUHUSU MAISHA YAKO YA KILA SIKU:

Tuangalie aina nyingine za huo utendaji kazi;


                  JAMBO LA TATU:

( 3 ) Madhabahu za nchi zinaweza kupitisha vita kwako inayotokana na makabila yaliyomo ndani ya nchi.

Yona 1:8 Ufunuo 13:1-2,7 Habakuki 3:9 Zekaria 11:10 Ufunuo 5:9

Kuna vita ndani ya nchi ambazo chanzo chake ni madhabahu za nchi kwa kutumia makabila yaliyomo ndani ya nchi yenu, kwahiyo swala la kujua idadi za makabila yaliyomo ndani ya nchi yenu na utendaji kazi wa hayo makabila ni jambo la msingi sana kulijua kiroho. Kwahiyo kuna vita kwenye maeneo mbalimbali ya maisha yako unazokutana nazo kila siku ambazo chanzo chake ni madhabahu za nchi kutumia makabila yaliyomo ndani ya nchi.

❌Je katika nchi unayoishi hizo madhabahu za miungu zilizomo ndani ya nchi zinatumia vita gani za makabila kuja kwenye maisha yako? Hakikisha kwamba unapambana kwenye maombi yako kupangua vita vyote unavyokutana navyo kutoka kwenye madhabahu za nchi kwasababu ya makabila yaliyomo ndani ya nchi.


                 JAMBO LA NNE:

( 4 ) Madhabahu za nchi zinaweza kuyafunga maisha yako kupitia viapo vinavyofanywa kwenye hizo madhabahu kwaajili ya nchi unayoishi.

1Waflme 8:31  Hesabu 30:2 Mathayo 23:20

🔵 Kuna watu wengi sana katika nchi maisha yao yamefungwa na viapo vilivyofanyika na vinavyofanyika ndani ya nchi kila siku kupitia madhabahu za nchi za miungu na viapo hivyo vinahusisha kuifunga nchi na kwasababu wewe unaishi ndani ya nchi unajikuta unadhurika na hivyo viapo vinavyofanyika kila siku kwa siri katika nchi yenu, kama hutakuwa mtu wa kuiombea nchi na kupambana na hizo madhabahu utajikuta maisha yako hayastawi ukiwa ndani ya nchi kutokana na hivyo viapo vya nchi.

❌Je unajifunguaga kila siku katika viapo vya madhabahu za nchi yenu? Hakikisha unapambana sana na viapo vya madhabahu za nchi yenu kila siku kwa maombi na kuyafungua maisha yako na maisha yenu ili uweze kuwa na maisha mazuri katika nchi unayoishi.


                  JAMBO LA TANO:

( 5 ) Sadaka zinazotolewa kwenye madhabahu za miungu za nchi yetu zinaweza kuyafunga maisha yako.

Ezra 3:2  Zaburi 118:27 Waamuzi 6:11,25-26

Kuna maisha ya watu ndani ya nchi yamefungwa na sadaka zilizotolewa kwenye madhabahu za nchi za miungu, na kuna watu wengi wanatoa sadaka kwenye madhabahu za nchi ili kuifunga nchi unayoishi na maisha ya nyie wananchi mliomo ndani ya nchi, hivyo hakikisha kwamba unapambana na jambo hili kwenye ulimwengu wa roho.

❌Je unafanya maombi ya kuharibu kila sadaka zilizotolewa kwenye madhabahu za miungu za nchi yenu zilizofunga maisha yako? Hakikisha unayafungua maisha yako kwenye hizo sadaka katika hizo madhabahu za nchi, pia hakikisha kwamba unakuwa mtiifu na mwaminifu katika kutoa Sadaka mbalimbali kwenye madhabahu ya Mungu katika Yesu Kristo kila wakati ili kupitia sadaka hizo unazotoa kwa Mungu hiyo madhabahu ya Mungu iweze kupambana na hizo madhabahu za nchi za miungu.

✔️ Tunaishia hapa kwa semina ya leo tukutane siku ya kesho ambapo tutaliangalia lango la Nafsi yako hakikisha kwamba unafanyia kazi somo hili kila siku kwa maombi yako. Nakuomba pia hakikisha unawashirikisha watu wengine na magroup mengine masomo haya ili wapokee Maarifa haya ya Neno la Mungu.


Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi:

Vodacom +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com



Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

          Samwel Kibiriti.

Mei 23, 2021

@Kibiriti2021

Karibu upokee Maarifa mbalimbali kwenye Vitabu nilivyoandika vya Neno la Mungu.

Wednesday, June 9, 2021

11:36 PM

 30-day seminar (Christ For All People Church- Mbeya).

DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM .

        Day 8 of the Seminar

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Praise be to Jesus Christ, the Son of God, let us unite in today's seminar. 


FIGHT AGAINST THE ALTARS OF THE COUNTRIES THAT CLOSED YOUR LIFE AND YOUR LIFE ( A ) .

Deuteronomy 12: 1-4

Having finished asking you 5 questions about the gate of the country you live in and guiding you how to pray in relation to your country I believe you have worked on those questions, today and tomorrow I want to pass you on in this matter of the altars of the country how they were involved in closing your life. There are millions of citizens in the country whose lives are confined to local altars.

The altars of the country are very much involved in capturing and imprisoning the lives of the people in the country because when you live in the spiritual world those altars have the right to arrest and imprison you if you do not know how to pray. And many countries in the world carry altars of the gods and not the altars of the living God in Jesus Christ, and because Christians have failed to build an altar to God wherever they live and work they have found their daily lives controlled spiritually by the altars of the countries in which they live.


You yourself are a witness there are so many things in your life that don't go the way you want and what God intended you to do because of those altars of the world, you work, you farm, you raise livestock, you study etc. but when you do an assessment you find things don't go very fast. by prayer, so realize that living in a land with altars to the gods will cause you great distress in your daily life.


PERFORMANCE OF THE ALTAR COUNTRIES ABOUT YOUR DAILY LIFE :

Let me show you a few spiritual things about the functioning of the altars of the nations involved in capturing and closing them and destroying your life. And because many Christians do not have a good relationship with the altar of God but have a good relationship with their church buildings they have found themselves attacked for life by the altars of the gods of the world without getting much help from the altar of God in Jesus Christ.


                 FIRST THING :

( 1 ) The altars of the country are responsible for your work in the country .

Psalm 104: 23 Judges 6: 11-32 Ecclesiastes 3: 13,22 Revelation 16: 7


I want you to know that the altars of the country where you live spiritually are very much related to your handicrafts that you do in the country as well as your works that you do in the country and this is something most people who live in the country do not realize but that is true. of the gods in your country that is why you do not get much benefit from your handicrafts but you continue to do it because you have no way of living if you do not do it even if you do not get the right profit.

There are many people in the country whose handicrafts they do every day are held and closed by the altars of the countries in which they live and thus instead of work being part of their happiness the work has turned and slavery to them is what you hear someone say this work is very tiring or I do not see this work any benefit to do with my employment or this job only hurts me even though I do it. All of this is due to the functioning of the altars in your country.


❌ To what extent have the altars of your country been involved in torturing you in your handicrafts? Make sure you go into the power of prayer to deal with the altars of the gods of the gods that have closed your handiwork that you do in the country and then open your handiwork in that country and after that make sure the area where you do your handiwork you build God Altar there of the hands and the altar of the living God in Jesus Christ then you will see your benefits and prosperity in life through those handicrafts you do in the world.


              SECOND THING :

( 2 ) The altars of the land can control you in living and serving your Purpose of Life .

Romans 9:11, Ephesians 1: 4 Genesis 11: 31-32, 12: 1-4


🔵 In the country you live in I want you to know that the altars of your gods in the spirit world have a large percentage to control you in living and serving God's purpose to create you and bring you here on earth, that's why look in your life if you live in purpose. your creation. Most people in the country are not in their creative purpose but they are living life without purpose which is why the cry of life being difficult does not live in their mouths.

When God created you He closed your life into your purpose of creation and when He brought you to earth God intended you to live that life for the rest of your life but unfortunately there are many things involved in keeping your purpose in the presence of the altar of the land you live in now instead of living your real life. today you are living a life that photocopy that is not yours is where now suffering and anxiety have become part of your life because you are out of your God-created purpose.


❌ To what extent have the altars of your country of origin adhered to your purpose of being created by God? Do you live and serve God's purpose for your life in the country you are in? Make sure you enter into a powerful prayer in beating down all the altars of the gods of the gods that held your creation purpose, command them to release you and let go of your purpose and also make sure you open your creation purpose on those altars of the land, and the creative purpose of your children and parents by the blood of Jesus and the name of Jesus Christ in the earth.

To find out more about your creative purpose find my book I HAVE CALLED THE THINGS CARRIED INTO YOUR GOD'S CREATION PURPOSE in the books I have taught you a great deal about the purpose is Tsh 5,000 (Five Thousand) almost get your own copy.


✔️ For today our seminar ends here let's meet tomorrow for the seminar where I will show you another performance of the altars of the country you live about your daily life in that country. I beg you to help me share these lessons with others and God will bless you for making this ministry so that more people will not continue to suffer and receive this knowledge of God's Word, send the lesson as it is without removing anything.


Contact me at the following numbers:

Vodacom +255 765 867574 (WhatsApp).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

By Email address is Pastorkibiriti@gmail.com



I am a Teacher of God's Word of Knowledge

         Samuel Kibiriti .

May 22, 2021

@ Kibiriti2021

Let's meet at tomorrow's seminar where God will serve us again as He did for you today.

11:20 PM

 Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

        Day 8 ya Semina

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Asifiwe Yesu Kristo mwana wa Mungu karibu tuungane katika semina ya siku ya leo. 

KUPAMBANA NA MADHABAHU ZA NCHI ZILIZOFUNGA MAISHA YAKO NA MAISHA YENU ( A ).

Kumbukumbu 12:1-4

Baada ya kumaliza kukuuliza maswali 5 kuhusu lango la nchi unayoishi na kukuongoza jinsi ya kuomba kuhusiana na nchi yenu naamini kwamba umefanyia kazi yale maswali, leo na kesho nataka nikupitishe katika jambo hili la madhabahu za nchi jinsi zilivyohusika kuyafunga maisha yako. Kuna mamilion ya wananchi waliomo ndani ya nchi ambao maisha yao yamefungwa katika madhabahu zilizomo ndani ya nchi.


Madhabahu za nchi zimehusika sana kuyakamata na kuyafunga maisha ya watu waliomo ndani ya nchi kwasababu unapoishi katika nchi kiroho hizo madhabahu ziko na uhalali kukukamata na kukufunga kama hutajua jinsi ya kuomba. Na nchi nyingi duniani zimebeba madhabahu za miungu wala sio madhabahu za Mungu aliye hai katika Yesu Kristo, na kwasababu wakristo wameshindwa kumjengea Mungu madhabahu kila mahali wanapoishi na kufanya kazi wamejikuta maisha yao ya kila siku yanadhibitiwa kiroho na hizo madhabahu za nchi wanazoishi.


Wewe mwenyewe ni shahidi kuna mambo mengi sana kwenye maisha yako hayaendi vile unavyotamani na vile Mungu alivyokukusudia yaende kwasababu ya hizo madhabahu za nchi, unafanya kazi, unalima, unafuga mifugo, unasoma n.k lakini ukifanya tathimini unakuta mambo hayaendi kwa haraka yanaenda taratibu sana hadi ulazimishe sana kwa maombi, hivyo tambua kwamba kuishi katika nchi yenye madhabahu za miungu utapata shida sana katika maisha yako ya kila siku.

UTENDAJI KAZI WA MADHABAHU ZA NCHI KUHUSU MAISHA YAKO YA KILA SIKU:


Ngoja nikuonyeshe mambo machache ya kiroho kuhusu utendaji kazi wa madhabahu za nchi zinavyohusika na kuyakamata na kuyafunga na kuyaharibu maisha yako. Na kwasababu wakristo wengi hawana mahusiano mazuri na madhabahu ya Mungu ila wako na mahusiano mazuri na majengo yao ya makanisa wamejikuta watu wa kushambuliwa kimaisha na madhabahu za miungu za nchi pasipo kupata msaada mkubwa sana kutoka  kwenye madhabahu ya Mungu katika Yesu Kristo.


                 JAMBO LA KWANZA:

( 1 ) Madhabahu za nchi zinahusika na kazi zako unazofanya ndani ya nchi.

Zaburi 104:23 Waamuzi 6:11-32 Mhubiri 3:13,22 Ufunuo 16:7


Nataka utambue kwamba madhabahu za nchi unayoishi kiroho zinahusika sana na kazi zako za mikono unazozifanya ndani ya nchi pia na kazi zenu mnazozifanya ndani ya nchi na jambo hili watu wengi mnaoishi katika nchi hamlitambui lakini huo ndio ukweli kazi zako unazofanya ndani ya nchi zimeshikiliwa kiroho na madhabahu za miungu zilizomo ndani ya nchi yenu ndio maana hakuna faida kubwa unayoipata katika kazi zako za mikono ila unaendelea kufanya kwasababu huna namna yoyote ya kuishi usipozifanya hata kama haupati faida inayoshahili.


Wako watu wengi ndani ya nchi kazi zao za mikono wanazofanya kila siku zimeshikiliwa na kufungwa na madhabahu za nchi walizomo na hivyo kusababisha badala ya kazi kuwa sehemu ya furaha kwao kazi zimegeuka na kuwa utumwa kwao ndio unasikia mtu akisema hii kazi inanichosha sana au hii kazi sioni faida yoyote ya kufanya pamoja na kuajiliwa kwangu au hii kazi inajitesa tu ingawa naifanya. Haya yote yanasababishwa na utendaji kazi wa hizo madhabahu zilizomo ndani ya nchi yenu.


❌ Je madhabahu za nchi yenu zimehusika kwa kiwango gani kukutesa katika kazi zako za mikono? Hakikisha unaingia katika maombi ya nguvu kuzishughulikia madhabahu za nchi za miungu zilizofunga kazi zako za mikono unazozifanya ndani ya nchi kisha fungua kazi zako za mikono katika hiyo nchi na baada ya hapo hakikisha eneo unalofanyia kazi zako za mikono unamjengea Mungu Madhabahu yake hapo na kuziunganisha kazi zako za mikono na madhabahu ya Mungu aliye hai katika Yesu Kristo ndipo utaona faida na kustawi kwako kimaisha kupitia hizo kazi za mikono unazofanya katika nchi.


              JAMBO LA PILI:

( 2 ) Madhabahu za nchi zinaweza kukudhibiti katika kuliishi na kulitumikia Kusudi lako la Maisha.

Warumi 9:11, Waefeso 1:4 Mwanzo 11:31-32, 12:1-4


🔵 Katika nchi unayoishi nataka ujue kwamba hizo madhabahu za nchi yenu za miungu katika ulimwengu wa roho zimehusika kwa asilimia kubwa sana kukudhibiti katika kuliishi na kulitumikia kusudi la Mungu la kukuumba wewe na kukuleta hapa duniani, ndio maana angalia katika maisha yako kama uaishi ndani ya kusudi lako la uumbaji. Watu wengi ndani ya nchi hawako kwenye kusudi lao la uumbaji ila wanaishi maisha wakiwa nje ya kusudi ndio maana kilio cha maisha kuwa magumu hakiishi katika vinywa vyao.


Maisha yako Mungu alipokuumba aliyafunga ndani ya kusudi lako la uumbaji na alipokuleta hapa duniani Mungu amekusudia uweze kuyaishi hayo maisha yako kwa kipindi utakachokuwepo duniani ila kwa bahati mbaya kuna mambo mengi yemehusika kulishika kusudi lako yakiwepo madhabahu ya nchi unayoishi ndio sasa badala ya kuyaishi maisha yako halisi leo unaishi maisha photocopy yasiyokuwa yako ndio hapo sasa kuteseka na kuhangaika kumekuwa sehemu ya maisha yako kwasababu uko nje ya kusudi lako la kuumbwa na Mungu.


❌ Je madhabahu za nchi yako unayoishi zimeshikilia kusudi lako la kuumbwa na Mungu kwa kiwango gani? Je unaishi na kulitumikia kusudi la Mungu kwenye maisha yako ndani ya nchi uliyopo? Hakikisha unaingia kwenye maombi ya nguvu katika kuzipiga madhabahu zote za nchi za miungu zilizoshikilia kusudi lako la uumbaji, ziamuru zikuachilie na kuachia kusudi lako na pia hakikisha unalifungua kusudi lako la uumbaji kwenye hizo madhabahu za nchi, na kusudi la uumbaji la watoto na wazazi wako lifungue kwa damu ya Yesu na jina la Yesu Kristo katika nchi.


Kufahamu mambo mengi kuhusu Kusudi lako la uumbaji tafuta kitabu changu nilichoandika kiitwacho VITU VILIVYOBEBWA NDANI YA KUSUDI LAKO LA KUUBWA NA MUNGU ndani ya vitabu nimefundisha maarifa makubwa sana kuhusu kusudi ni Tsh 5,000 ( Elfu Tano ) karibu ujipatie Nakala yako.


✔️ Kwa leo semina yetu inaishia hapa tukutane siku ya kesho ya semina ambapo nitakuonyesha utendaji mwingine wa madhabahu za nchi unayoishi kuhusu maisha yako ya kila siku katika hiyo nchi. Nakuomba sana nisaidie kuwashirikisha watu wengine masomo haya na Mungu atakubariki kwa kuifanya huduma hii ili watu wengi wasiendelee kuteseka wapokee maarifa haya ya Neno la Mungu, ulitume somo kama lilivyo bila kuondoa chochote.


Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi:

Vodacom +255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel +255 785 855785

Tigo +255 673 784197

Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com



Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

         Samwel Kibiriti.

Mei 22, 2021

@Kibiriti2021

Tukutane katika semina ya siku ya kesho ambapo Mungu atatuhudumia tena kama alivyokuhudumia siku ya leo.

Tuesday, June 8, 2021

5:09 AM

 30-day seminar (Christ For All People Church- Mbeya).

DEALING WITH SPIRITUAL GATES THAT AFFECT YOUR DAILY LIFE SYSTEM .

         Day 7 of the Seminar.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Praise the Lord Jesus Christ, may the Son of God continue with our seminar.

FIGHTING THE GATE OF THE COUNTRY YOU LIVE IN ( C ) .

Matthew 12:40 Nahum 3:13 Jonah 1: 8

In yesterday's seminar we looked at the Second question and today I would like to introduce you to other questions about the country you live in;


                 QUESTION THREE :

( 3 ) What are the gates of your country passing and importing into the country? .

Nahum 3:13 Lamentations 4:12 Nehemiah 13:19

I want to ask you in the gates of your country what they pass through and import what things in the country and the lives of citizens? Many of the gates of the world, if you pursue them spiritually, bring in very bad things for the country and these things have closed the lives of the people living in the country, and the church is asleep and does not pray for the gates of the country. the day you pray for the gates of your land before God.

Make sure you hand over the gates of your country to God so that Satan and his enemies will not be able to use them and close the country and your lives, citizens.


                QUESTION FOUR :

( 4 ) Who is your country spiritually? .

2 Samuel 3:12 Psalm 33:12 2 Kings 17: 24-276

Who owns the country in which you live spiritually? I know you have never wondered and pondered this question and its consequences you live in a world you do not know who you are spiritually and as a result your spiritual landlord has been guiding your life even if you do not want to. As you trace into the spirit world many foreign gods are not the lands of God in Jesus Christ and you live in a land that belongs to the gods.

Contemplate this notion as you interact with your neighbors. The question is not to be born in a country or to have a citizenship ID I want you to know that in the spirit world the country can be God or gods, so make sure you go into prayer and pray for your country and deliver it into the hands of the devil / gods and then enter the country into God's hands so that God can take care of your country and your daily life.


             QUESTION FIVE :

( 5 ) What are the presidential seats in your country carrying for the country? .

2 Samuel 21: 1 Hebrews 4:16

The presidential seat in the country contains various spiritual things I want to ask you in the country where you live what the chair of your presidency is carrying for the country and your life? I want you to know that there is a difference between the President and the presidency because the president at the end of his term of office leaves but the presidency still remains in your country.

How many people who live in the country realize what your presidential seat is carrying? As you trace the many problems in the country and the lives of the people that afflict them from generation to generation that occur in the presidency of their country. The church does not have a system for praying for the presidency before God and as a result the country through difficult times I ask you to pray earnestly for the presidency in your country and to remove all unworthy things carried in your presidency and hand over the presidency under God's rule. .

You may have a good president with a very big vision for your country and your life but spiritually he was hindered by the things in the presidency that he uses to rule that is why I urge you to make sure you pray for the presidency in your country.

✔️ For today I ask you to reflect on these questions about your country and pray before God, to meet us tomorrow where we will still continue with this area of ​​the country. Help me share these lessons with others and in the other groups you are in.

Contact me at the following numbers:

Vodacom M-PESA + 255 765 867574 (WhatsApp).

Airtel Money +255 785 855785.

Tigo Money +255 673 784197.

By Email address is Pastorkibiriti@gmail.com



I am a Teacher of God's Word of Knowledge

         Samuel Kibiriti .

May 21, 2021

Mbeya Tanzania.

@ Kibiriti2021

Welcome to tomorrow's seminar where we will continue to receive knowledge of God's Word

Monday, June 7, 2021

9:41 PM
Semina ya siku 30 ( Christ For All People Church- Mbeya ).

KUYASHUGHULIKIA MALANGO YA KIROHO YANAYOGUSA MFUMO WAKO WA MAISHA YA KILA SIKU.

         Day 7 ya Semina.

Senior Pastor Samwel Kibiriti.

Bwana Yesu Kristo asifiwe karibu mwana wa Mungu tuendelee na semina yetu.

KUPAMBANA NA LANGO LA NCHI UNAYOISHI ( C ).

Mathayo 12:40  Nahumu 3:13  Yona 1:8

Katika semina ya siku ya jana tuliangalia swali la Pili naomba leo nikupitishe katika maswali mengine kuhusu nchi unayoishi;


                 SWALI LA TATU:

( 3 ) Malango ya nchi yenu yanapitisha na kuingiza vitu gani katika nchi?.

Nahumu 3:13  Maombolezo 4:12 Nehemia 13:19

Nataka nikuulize katika malango ya nchi yenu yanapitisha na kuingiza vitu gani katika nchi na maisha ya wananchi? Malango mengi ya nchi ukiyafuatilia rohoni yanaingiza vitu vibaya sana kwaajili ya nchi na vitu hivyo vimeyafunga maisha ya wananchi wanaoishi katika nchi, na kanisa limelala haliombei malango ya nchi na hivyo maadui hupitisha vitu vyao vya uovu katika nchi, nakuomba wewe kanisa amka na uhakikishe kwamba kila siku unayaombea malango ya nchi yenu mbele za Mungu.

Hakikisheni mnayakabidhi malango ya nchi yenu kwa Mungu ili Shetani na maadui wasiweze kuyatumia na kuifunga nchi na maisha yenu wananchi.


                SWALI LA NNE:

( 4 ) Je nchi yenu niya nani kiroho?.

2Samwel 3:12  Zaburi 33:12 2Waflme 17:24-276

Nchi unayoishi niya nani kiroho? Najua hujawahi kujiuliza na kutafakari hili swali na matokeoa yake unaishi katika nchi usiyojua niya nani kiroho na matokeo yake mwenye nchi yenu rohoni amekuwa anayaongoza maisha yako hata kama hutaki. Unapofuatilia kwenye ulimwengu wa roho nchi nyingi niza miungu migeni sio nchi za Mungu katika Yesu Kristo na kuishi katika nchi ambayo niya miungu utambue wazi kwamba hiyo miungu ndio itakayohusika na nchi na maisha ya wananchi waliomo ndani yake.

Tafakari sana hili swali je nchi yenu niya nani kiroho? Swala sio kuzaliwa katika nchi au kuwa na kitambulisho cha uraia nataka ujue kwamba katika ulimwengu wa roho nchi inaweza kuwa ya Mungu au miungu, hivyo hakikisha kwamba mnaingia kwenye maombi na kuiombea sana nchi yenu na kuitoa kwenye mikono ya shetani/miungu na kisha kuingiza nchi kwenye mikono ya Mungu ili Mungu aweze kuisimamia nchi yenu na maisha yenu wananchi ya kila siku.


             SWALI LA TANO:

( 5 ) Je kiti cha Urais katika nchi yenu kimebeba vitu gani kwaajili ya nchi?.

2Samwel 21:1  Waebrania 4:16

Kiti cha urais katika nchi kimebeba vitu mbalimbali vya kiroho nataka nikuulize katika nchi unayoishi kile kiti cha urais wenu kimebeba vitu gani kwaajili ya nchi na maisha yenu? Nataka ujue kwamba kuna tofauti ya Rais na kiti cha Urais kwasababu rais akimaliza muda wake wa uongozi huondoka ila kiti cha urais bado kinabakia katika nchi yenu.

Ni watu wangapi ambao mnaoishi katika nchi mnatambua kiti chenu cha urais kimebeba vitu gani? Unapofuatilia matatizo mengi katika nchi na maisha ya wananchi yanayowatesa toka kizazi hadi kizazi yako yanayotokea katika kiti cha urais cha nchi yao. Kanisa halina utaratibu wa kuombea kiti cha urais mbele za Mungu na matokeo yake nchi kupitia nyakati ngumu nakuomba uwe unakiombea sana kiti cha urais katika nchi yenu na kupangua vitu vyote visivyofaa vilivyobebwa katika kiti cha urais wenu na kukabidhi hicho kiti cha urais chini ya utawala wa Mungu.

Mnaweza kuwa na rais mzuri mwenye maono makubwa sana kwaajili ya nchi yenu na maisha yenu lakini kiroho akakwamishwa na vitu vilivyopo kwenye kiti cha urais anachokitumia kutawala ndio maana nasisitiza kwamba hakikisheni mnakiombea sana kiti cha urais katika nchi yenu.

✔️ Kwa siku ya leo naomba utafakari maswali haya kuhusu nchi yenu na kuomba mbele za Mungu, tukutane siku ya kesho ambapo bado tutaendelea na eneo hili la nchi. Nisaidie kuwashirikisha wengine masomo haya na kwenye magroup mengine uliyopo.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa namba hizi:

Vodacom M-PESA+255 765 867574 ( WhatsApp ).

Airtel Money +255 785 855785.

Tigo Money +255 673 784197.

Kwa Email address ni Pastorkibiriti@gmail.com




Mimi ni Mwalimu wa Neno la Mungu la Maarifa

          Samwel Kibiriti.

Mei 21, 2021

Mbeya Tanzania.

@Kibiriti2021

Karibu katika semina ya siku ya kesho ambapo tutaendelea kupokea maarifa ya Neno la Mungu.

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...