Post Top Ad

Post Top Ad

Saturday, July 29, 2017

3:35 AM

MAOMBI YA KUMKUMBUSHA MUNGU.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.


Shalom karibu tena tuendelee kujifunza somo hili la aina tofauti za maombi.



{ KIPENGELE CHA TISA }.

Kuna Maombi ya Kumkumbusha Mungu.

Haya ni maombi pia ambayo unatakiwa umuombe Mungu yaani ni mfumo wa kumuomba Mungu kwa kumkumbusha kwa yale aliyokuahidi kwamba atakutendea kwenye maisha yako lakini amekawia kukupatia.

  Inawezekana kabisa ni kweli Mungu amekuahidi ahadi nyingi kwamba atakutendea kwenye maisha yako lakini bado hizo ahadi hazijadhihilika katika maisha yako, kwahiyo unachotakiwa ni kumwendea Mungu kwa mfumo huu wa maombi ya kumkumbusha kwamba Mungu uliniahidi kwamba utanitendea jambo Fulani lakini bado hujanitendea leo nakuja mbele zako kukukumbusha Baba ili unitimilizie jambo hilo kwenye maisha yangu.

                               Isaya 43

26 Unikumbushe; na tuhojiane; eleza mambo yako, upate kupewa haki yako.

   Mungu anasema tumkumbushe, sasa anaposema kwamba tumkumbushe haina maana kwamba amesahau Mungu hapana ila anachotaka ni kuona kwamba unaouhitaji ndani ya moyo wako wa kumuona Mungu anatimiza zile ahadi alizokueleza/kukuahidia kwahiyo unapomkumbusha Mungu maana yake anaona kwamba kumbe ndani ya moyo wako unamtaka yeye akitimizie hizo ahadi kwenye maisha yako.

    Nitahitaji usome kitabu cha MALAKI 3:13-18 utaona watu waliokuwa wanamtumikia Mungu wanasemezana maneno magumu sana mbele za Mungu kwamba hakuna faida ya kumtumikia Mungu ndipo akawajibu na kuwaambia kwamba “Ndipo wale waliomcha BWANA waliposemezana wao kwa wao. Naye BWANA akasikiliza, akasikia; na kitabu cha Ukumbusho kikaandikwa mbele zake, kwa ajili ya hao waliomcha BWANA, na kulitafakari jina lake”.

Unaona kule mbinguni Mungu anacho kitabu cha Ukumbusho kwahiyo unapomuomba Mungu maombi haya ya kumkumbusha maana yake unamuomba Mungu arudi kwenye hicho kitabu chake cha ukumbusho na aangalie zile ahadi alizokuahidia kwamba atakutendea kwenye maisha yako.

  Ukisoma pia kwenye kitabu cha Isaya 38:1-6 wakati Hezekia alipokuwa mgonjwa na kupewa taarifa kwamba atakufa aligeuka ukutani na kumkumbusha Mungu na Mungu akamsikia na kukumbuka mambo aliyowahi kuyatenda huko nyumba kwenye ufalme wake.


     Ndio maana kuna kipindi cha maisha kinafika unachotakiwa ni kuingia kwenye maombi haya ya kumkumbusha Mungu kwamba Mungu kumbuka mambo niliyofanya kwenye ufalme wako na Mungu ataenda kwenye kitabu hicho cha ukumbusho na kuangalia utumishi wako naye atakujibu na kukutendea au kukuvusha mahali pagumu sana kimaisha.

   Mungu akubariki sana tukutane tena siku ya kesho.

kwa mawasiliano nami utanipa kwa simu hizi:

vodacom +255 765 867574.

tigo          +255 673 784197.

Airtel       +255 785 855785.

Kwa Email ni  Pastorkibiriti@gmail.com

July 29, 2017.


                     Mwalimu Samwel Kibiriti.


Friday, July 28, 2017

12:56 AM
LEO IJUMAA TAREHE 28/07/2017 SEMINA YETU INAINGIA SIKU YA TANO HAPA BOMA HAI KILIMANJARO.

KARIBU USHIRIKI NASI KATIKA SEMINA HII HAPA KATIKA HEMA YA HUDUMA YA FIRE FIRE UKOMBOZI KARIBU NA SHULE YA SEKONDARY SHELELA.

AU FUATANA NAMI KATIKA SEMINA HII KUPITIA UKURASA WANGU WA FACEBOOK AMBAO NI Samwel Kibiritiministry

UBARIKIWE SANA NA IJUMAA NJEMA SANA KWAKO.
12:48 AM

MAOMBI YA ULINZI.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

Bwana Yesu Kristo asifiwe sana.

karibu tena ndani ya blog hii uweze kupokea maarifa haya ya kiroho.




{ KIPENGELE CHA NANE }

Kuna Maombi ya Ulinzi.

Haya ni maombi ambayo unatakiwa sana kumuomba Mungu kwa sababu katika dunia hii tunayoiishi tumezungukwa na adui yetu mkuu shetani pamoja na wajumbe/ vibaraka vyake ambao ni wachawi, waganga wa kienyeji, mapepo, majini, mizimu, maadui n.k 

    kwahiyo ni lazima umuombe Mungu kila siku ili akulinde na kulinda familia yako/yenu, kuwalinda watoto wako, kulinda mali zako n.k

                        AYUBU 1

9 Ndipo Shetani akamjibu BWANA, na kusema, je! Huyo Ayubu yuamcha BWANA bure?

10 Wewe hukumzingira kwa ukigo/ukuta pande zote, pamoja na nyumba yake, na vitu vyote alivyo navyo? Kazi za mikono yake umezibarikia, nayo mali yake imeongezeka katika nchi.

Hapa unayakuta ni mazungumzo kati ya Mungu na Shetani wakati Shetani ametokea huku duniani Mungu akamuuliza Shetani kwamba je amemuona huyo mtumishi wake Ayubu, na Shetani akamjibu Mungu kwamba amemzunguzia ulinzi Ayubu kwahiyo kutokana na ule ulinzi kwa Ayubu na nyumba yake na mali zake ulimfanya asiweze kumshambulia na kumpiga Ayubu.

  Kwahiyo sasa unamuona Shetani anamshawishi Mungu auondoe ule ulinzi wake kwa Ayubu na nyumba yake na mali zake ili aweze kumshambulia na kumpiga, ndio maana Mungu alipomuondolea Ayubu ule ulinzi wake akapata nafasi ya kumpiga na kumshambulia.

   Kwahiyo sasa unatakiwa sana umuombe Mungu ulinzi wake katika maeneo yote ya maisha yako yaani muombe Mungu akulinde wewe mwenyewe, alinde mali zako, alinde watoto wako, alinde wazazi wako, alinde nyumba yako, ayalinde masomo yako n.k ili shetani na wachawi na waganga wa kienyeji na mapepo na majini na roho za mizimu zisiweze kukushambulia.

   Hakikisha usiku na mchana unamuomba Mungu ulinzi wake kwenye kila eneo la maisha yako.

    Kwa mawasiliano nami utanipata kwa simu namba hizi:


Vodacom +255 765 867574.


Tigo         +255 673 784197.


Airtel       +255 785 855785.


kwa Email utanipata kwa   Pastorkibiriti@gmail.com


blogsport: Samwel Kibiritiministry.blogsport.com


July 28, 2017.


Mwalimu Samwel Kibiriti.




                                

Thursday, July 27, 2017

6:51 AM

SEMINA YA NENO LA MUNGU.

KARIBU SANA KATIKA SEMINA HAPA BOMA, HAI, KILIMANJARO.



Bwana Yesu asifiwe sana mwana wa Mungu,

ninayo semina ya siku nane { 8 } hapa katika mji wa bomang'ombe, wilaya ya Hai mkoa wa Kilimanjaro, katika nchi ya Tanzania, kuanzia tarehe 23 hadi 30/07/2017.

Semina hii ninairusha moja kwa moja Live kila siku kuanzia saa 11 jioni katika ukurasa wangu wa Facebook ambao ni   "Samwel Kibiritiministry".

Ungana nasi kwa njia ya maombi yako kuombea semina hii.

Somo la Semina ambalo Mungu alinipatia linakichwa kinachosema  "KWANINI MTU ALIYEOKOKA ANAHITAJI KUFUNGULIWA?". hili ni somo la msingi sana kwa kila mtu aliyeokoka kulifahamu.

Mungu Baba ayahifadhi maisha yako naya uzao wako milele.

                        Mwalimu wa Semina 
                             Samwel Kibiriti.

Tuesday, February 28, 2017

10:22 PM

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.




Nakusalimu katika jina la Yesu Kristo karibu tena leo katika somo letu hili ili upokee maarifa.

KIPENGELE CHA SABA.

KUNA MAOMBI YA KUDAI HAKI ZAKO MBELE ZA MUNGU.

Huu ni mfumo mwingine wa maombi ambayo unaweza kuyafanya mbele za Mungu ambayo ni maombi ya kudai zile haki zako ambazo shetani na ufalme wake wamezizuia ili usiwe nazo.

   ziko haki zako nyingi sana ambazo kwenye ulimwengu wa roho shetani inawezekana kabisa amekuibia na kukufichia, ambazo sasa unatakiwa uanze kuzidai na kuzirudisha.

ngoja nikuonyeshe kwa mfano ili uweze kunielewa.

{ i } Uzima na Uponyaji ni haki yako kama ni mtoto wa Mungu, soma Yakobo 5:13-15, Isaya 53:5, 1Petro 2:24.

{ ii } Kuwa na Amani na furaha ni haki yako, soma Zaburi 122:7,8 119:165, Malaki 2:5

{ iii } Kuolewa na kuoa ni haki yako, soma Isaya 34:14, Mwanzo 2:18

{ iv } Kuzaa watoto kwenye ndoa yako ni haki yako, soma Kutoka 23:26, Zaburi 127:3

{ v } Kutokuharibika kwa mimba ni haki yako, soma Kutoka 23:26


{ vi } Kujifungua pasipo kufanyiwa operesheni ni haki yako, Soma Isaya 66:9

{ vii } Kufanikiwa kiuchumi ni haki yako, soma Waefeso 1:3, 2Wakorintho 8:9, Kumb 8:18


{ viii } Kuwa na ulinzi wa Mungu kila siku ni haki yako, soma 1Petro 1:5

{ ix } Kufanikiwa kibiashara ni haki yako, soma Isaya 48:17, Zaburi 32:8, Kumb 28:5,12

{ x } Kuishi maisha marefu ni haki yako, soma Ayubu 5:26, Kutoka 23:26, Zekaria 8:4  n.k

hizo ni baadhi tu ya haki zako ambazo Mungu anakutaka uzipate kwenye maisha yako wewe ukiwa kama mtoto wake.

je wewe unazo hizi haki zako kwenye maisha yako? au tayari shetani na ufalme wake wa giza wameshakunyanganya haki zako hizo? kama umeshapokonywa hizi haki zako na hauko nazo kwenye maisha yako ni lazima uingie kwenye maombi na kumuomba Mungu ili akurudishie hizo haki zako kwenye maisha yako.

kwa mawasiliano nami utanipata kwa;

 simu za mkononi ni

vodacom 0765 867574
Tigo   0673 784197
Airtel  0785 855785

kwa Email ni Pastorkibiriti@gmail.com



 

mimi ni mwalimu Samwel Kibiriti.


unaweza kujipatia kitabu chako cha somo hili la AINA TOFAUTI ZA MAOMBI kipo wasiliana nami kwa simu namba hizo au kwa Email hiyo, naweza pia kukutumia mahali popote pale ulipo duniani.

           @kibiriti 2017, Marchi 1 
9:31 PM

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.




Shalom wana wa Mungu karibu sana ndani ya darasa kwa siku hii ya Leo. Naamini utapata maarifa Leo tena.


{ KIPENGELE CHA SITA }.

KUNA MAOMBI YA KUNG'OA KILICHOPANDWA NA SHETANI KWENYE MAISHA YAKO.

Haya ni maombi ambayo yanahusika na kung'oa vitu au mbegu za uovu zilizopandikizwa kwenye maisha yako na shetani na vitu hivyo hukutesa kwenye maisha yako.

Katika Ulimwengu wa roho upande wa giza kuna vitu vingi sana ambavyo havifai wanavyowapandikizia wanadamu kwenye miili yao na nafsi zao,

Unaweza kumkuta mtu amepandikiziwa roho mbalimbali mfano magonjwa, matatizo, mikosi, madeni, kushindwa, ulevi, uzinzi/uasherati, tabia mbaya n.k, hizi ni baadhi tu ya roho ambazo unaweza kupandikiziwa na zinakutesa sana sana kwenye maisha yako.

                                        MATHAYO 15

"13 Akajibu, akasema, kila pando asilolipanda Baba yangu wa mbinguni litang'olewa"
.
Unamuona Bwana Yesu anasema kwamba kila pando ambalo hajalipanda Baba yake wa mbinguni lazima ling'olewa, hii ikiwa na maana kwamba yako mapando ambayo yamepandikizwa na shetani ndani ya mtu, na yanatakiwa kung'olewa kwa njia ya maombi.

                                     MATHAYO 13

"25 Lakini watu walipolala, akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake".

Unaona kwamba shetani anaweza kupanda vitu vyake katikati ya maisha ya mwanadamu.

Ni kuulize wewe umepandikwa vitu gani maishani mwako na shetani? Au shetani amewapandikizia vitu gani watoto wako? Au amepandikiza nini kwenye familia na ukoo wenu?

Unaona kwamba unayokazi ya kumuomba Mungu na kung'oa chochote kile kilichopandikizwa ndani yako na shetani, wachawi, waganga wa kienyeji, roho za mizimu, maadui n.k

Kwa Leo naishia hapa tukutane siku ya kesho tena tukiendelea na somo hili.

Kwa mawasiliano nami utanipata kwa simu

Voda 0765 867574.

Tigo 0673 784197.

Airtel 0785 855785.


KAULI MBINU MWAKA 2017.

( 1 ) Acha dhambi.

( 2 ) Yesu Kristo anakuja.

( 3 ) Ishi katika maisha ya Utakatifu kila siku.





Mimi ni mwalimu Samwel Kibiriti Rafiki yako katika Kristo Yesu.


                                   @Kibiriti 2017, February 7.

Monday, February 6, 2017

9:01 AM

AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.



        AINA TOFAUTI ZA MAOMBI.
               

Bwana Yesu Asifiwe Rafiki yangu katika Kristo Yesu. Karibu tena siku hii ya Leo ndani ya darasa hili la kupokoea Maarifa.

              { KIPENGELE CHA TANO }

Leo nataka tusongee mbele kidogo katika somo hili tuone Aina ya tano ya Maombi ambayo unatakiwa uyaombe.


KUNA MAOMBI YA KUMUULIZA MUNGU.


Huu ni mfumo mwingine wa maombi ambayo unatakiwa uyafanye mbele za Mungu, yaani unafanya maombi ya kumuuliza Mungu.

Wakristo wengi huwa hawafanyi maombi ya kumuuliza Mungu. Iko faida kubwa sana ya kufanya maombi ya mfumo huu wa kumuuliza Mungu
Ni kwanini ufanye maombi ya mfumo huu wa kumuuliza Mungu?

"Tunafanya maombi haya ya kumuuliza Mungu kwa sababu yako mambo mengi yasiyofaa yanayotuandama kwenye maisha yetu, ambapo hatujuia chanzo cha hayo matatizo au hayo mambo, sasa ni lazima tumwendee Mungu Baba kwa mfumo wa maombi haya kumuuliza kwamba Mungu ni kwanini kuna tatizo hili kwenye maisha yangu? Naye atakujibu na kukueleza chanzo chake."

Ngoja nikuonyeshe mifano ya watu wawili waliofanya maombi ya mfumo huu wa kuuliza,

                         Mfano wa Kwanza:

                               MWANZO 25

21 "Isaka akamwomba BWANA kwa ajili ya mke wake, maana alikuwa tasa. Naye BWANA akamwitikia, na Rebeka mkewe akachukua mimba".
22 "Watoto wakashindana tumboni mwake. Naye akasema, Ikiwa ni hivi, kuishi kwanifaa nini? Akaenda KUMWULIZA BWANA".
23 "BWANA akamwambia, Mataifa mawili yako tumboni mwako, Na kabila mbili za watu watafarakana tangu tumboni mwako. Kabila moja litakuwa hodari kuliko la pili, Na mkubwa atamtumikia mdogo".

Hapa unamuona Rebeka alipopatwa na shida ya mimba yake akaenda kumuuliza BWANA, yaani alifanya Maombi haya ya kumuuliza Mungu, na alimuuliza kwamba ni kwanini ile mimba inamsumbua. Na Mungu akamweleza sababu ya mimba hiyo kumsumbua na kumtesa.

Je wewe kuna jambo gani linalokutesa ambalo hujui chanzo cha tatizo hilo?

                          Mfano wa pili;

                          1 SAMWEL 23

2 "Basi Daudi akamwuliza BWANA, kusema, Je! Niende nikawapige hao Wafilisti? Naye BWANA akamwambia Daudi, Nenda ukawapige Wafilisti, na kuuokoa Keila".

Unamuona mfalme Daudi baada ya kuletewa taarifa kwamba Wafilisti wamevamia mji wa Keila na kuiba nafaka za watu, kabla hajaenda kupigana nao alichofanya Daudi ni kwenda Kumuuliza BWANA kwamba Je aende kupigana na Wafilisti au asiende? Na Mungu akamjibu na kumwambia aende kwa sababu atawashinda hao maadui zake.

Inawezekana na wewe iko vita kwenye maisha yako kwenye Ndoa, kazi, biashara, elimu, afya, uchumi, huduma n.k na huelewi chanzo cha hiyo vita sasa unachotakiwa ni wewe kwenda kwa mfumo huu wa maombi na kumuuliza Mungu kwamba "Ni kwanini vita hii imeinuka kwangu? Au kwanini napigana vita na Mimi sipati ushindi?" Ukimuuliza Mungu atakujibu na kukueleza chanzo cha hiyo vita na kukupatia mbinu za kuishinda hiyo vita.

Sijajua wakati unasoma somo hili uko katika hali gani ya kimaisha? Inawezekana yako mambo mengi sana ambayo yanakuandama kwenye maisha yako lakini hujui chanzo cha mambo hayo na umeomba lakini hujapata majibu kamili,

Sasa nakushauri katika Kristo Yesu nenda mbele za Mungu kwa mfumo wa maombi haya ya kumuuliza Mungu, kuhusu chanzo cha hayo matatizo hayo mambo hayo na Mungu atakujibu na kukueleza chanzo chake na atakupatia njia ya kufanya.
Kwa Leo naishia hapa tukutane siku ya kesho, fanyia kazi somo hili la Leo.

*                       Nataka nikueleze jambo hili kwamba mwisho wa wiki hii nitatoa kitabu cha somo hili la AINA TOFAUTI ZA MAOMBI ambapo nitaingia kwa undani sana, na kufundisha Aina nyingi sana za maombi ambayo unatakiwa uyafahamu na kumuomba Mungu."

Neema ya Mungu Baba ikuhifadhi.
Kwa mawasiliano nami utanipata kwa simu hizi

Voda 0765 867574
Tigo 0673 784197
Airtel 0785 855785

Asante sana kwa kujifunza somo hili.


mimi ni mwlm Samwel Kibiriti.

@Kibiriti 2017, February 6.

Featured Post

JINSI MISINGI YA VIZAZI INAVYOWEZA KUKAMATA MAISHA YAKO.

Fahamu kwamba misingi ni chanzo au asili au chimbuko la mtu. Na msingi wako wa vizazi unatokana na ukoo wako na kabila lako.      ...